November 28, 2015


Uongozi wa klabu ya Arsenal imeingia matatani na wanamazingira wa England ambao wamepinga kitendo cha timu yake kusafiri kwa dakika 14 leo wakati wakienda kuivaa Norwich katika mechi ya Ligi Kuu Engaland itakatopigwa kesho.


Kundi hilo la wanamazingira ambalo liliwahi kuingia mzozo na Arsenal mwaka 2012 baada ya kusafiri na ndege kwa maili 100 tu, limesema huo ni uharibibu mkubwa wa mazingira.

Hata hivyo, Kocha Mkuu, Arsene Wenger amesema wasingeweza kusafiri kwa basi kwa kuwa wangekutana na vizuizi vingi vya barabara kwa kuwa iko katika matengenezo.


Wenger anaamini usafiri wa basi, ungechangia uchovu kwa wachezaji wake hivyo ndege licha ya kuwa ni sehemu fupi kwa maana ya umbali, ndiyo ulikuwa usafiri sahihi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic