March 17, 2016



Beki kisiki wa zamani wa wa Manchester United, Jaap Stam amesema hana urafiki na kocha wake wa zamani, Alex Ferguson.

Lakini Stam raia wa Uholanzi akasisitiza, hana matatizo wala kinyongo na Ferguson ingawa uondoka yake katika klabu haikuwa ya kiungwana.

“Wakati huo sikufurahia, haikuwa vizuri namna alivyoniondoa. Lakini yale yamepita na sasa sina tatizo naye,” alisema Stam aliyekuwa mmoja wa mabeki maarufu wa kati duniani wakati akiichezea Man United na baadaye AC Milan.



Stam sasa ana umri wa miaka 43, alikataa kwenda Liverpool na kujiunga na Man United ambayo alifanikiwa kubeba ubingwa wa England mara tatu ukiwemo ule ushindi wa kihistoria wa mwaka 1999 wakati Man United ilipobeba ubingwa wa England, Ligi ya Mabingwa Ulaya na ubingwa wa Dunia.





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic