October 1, 2016


Wachezaji sita wa Real Madrid wameitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Hispania na kuweka rekodi.

Takribani miaka 13 sasa, haiku rahisi wachezaji wengi wa Madrid kuitwa kwa wingi lakini safari hii Kocha Julen Lopetegui kwaida sita timu hiyo maarufu kama Los Bloncos.

Sita walioitwa na Lopetegui ni Isco, Alvaro Morata na Lucas Vazquez kwa ajili ya ushambulizi, halafu Nacho, Sergio Ramos na Dani Carvajal katika ulinzi.

Wachezaji hao ni kwa ajili ya maandalizi ya mechi mbili, kwanza Italia halafu Albania.

KIKOSI CHA HISPANIA 2003

Mara ya mwisho wachezaji sita wa Madrid kuitwa kwa wakati mmoja ilikuwa mwaka 2003 walipoitwa akin Iker Casillas, Ivan Helguera, Raul Bravo, Michel Salgado, Guti na Raul.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic