November 22, 2016


Shirikisho la Soka la Sweden (SvFF) limetangaza kutengenezwa kwa sanamu maalum la mshambuliaji nyota wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic.

Zlatan ni mchezaji wa timu ya taifa ya Sweden na nahodha, lakini ni Mswidi aliyeshinda tuzo ya mwanamichezo bora wa Sweden kwa miaka 10 mfululizo.

Sanamu lake litawekwa nje ya Friends Arena katika jiji la Stockholm.

Hali hiyo ni kuonyesha kuthamini mchango wake akiwa na timu ya taiga ya Sweden lakini kuwasaidia wanamichezo chipukizi kuhakikisha wakiwa na hamu ya kupata mafanikio.

Zlatan ambaye sasa ana umri wa miaka 36, akiwa na timu ya taifa ya Sweden amecheza mechi 114 na kufunga mabao 62. Alitangaza kustaafu baada ya michuano ya Euro iliyofanyika nchini Ufaransa, hivi karibuni.



TAKWIMU ZAKE
KLABU ALIZOPITIA: Malmo, Ajax, Juventus, Inter, Barcelona, AC Milan, PSG, Manchester United
MECHI: 646; 
MABAO: 381
MECHI TIMU YA TAIFA: 116; 
MABAO: 62

MAKOMBE: 2009/10 La Liga, 4x Serie A (Mara tatu akiwa na Inter, Mara moja na AC Milan), 4x Ligue 1, 2x Eredivisie, 2010 FIFA Club World Cup, 2010 UEFA Supercup

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic