February 23, 2017

RUVU SHOOTING


Kikao cha Bodi ya Kusimamia na Kuendesha Ligi, kiliketi mwanzoni mwa wiki hii na kufanya tathmini ya mambo mbalimbali yaliyotokea kwenye michezo mbalimbali ya mpira wa miguu kwa michuano yote – Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.

Haya haya ndiyo yaliyojiri katika kila mchezo.


Mechi namba 173 (Ruvu Shooting vs Azam). Klabu ya Ruvu Shooting iandikiwe barua kuhusu ubovu wa uwanja wake eneo la kuchezea (pitch) ambapo kuna mashimo, hivyo wafanyie marekebisho.

Ligi Daraja la Kwanza
Mechi namba 49 (Polisi Morogoro vs Kinondoni Municipal Council FC). Klabu ya Polisi Morogoro imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika 20, kitendo ambacho ni kinyume na Kanuni ya 14(9) ya Ligi Daraja la Kwanza. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(48) ya Ligi Daraja la Kwanza.

Mechi namba 52 (Mbeya Warriors vs Njombe Mji). Mchezaji Boniface S. Nyagawa wa Mbeya Warriors amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kutoa lugha ya matusi kwa Mwamuzi Msaidizi Namba Moja, tukio lililosababisha atolewe kwenye benchi kwa kadi nyekundu. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 37(7).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic