October 20, 2017

MABARA

Kiungo wa Azam FC, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na mshambuliaji, Mbaraka Yusuph wameingia katika vita ya kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Septemba ambayo hutolewa kila mwezi klabuni hapo.

Majina hayo ya wachezaji wa Azam yamependekezwa na viongozi wa timu hiyo akiwemo kipa wa kigeni Razark Abalola raia wa Ghana miongoni mwa wachezaji watatu walioingia katika kinyang’anyiro hicho. 

Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffari Idd alisema kuwa, jopo la viongozi wamepitisha majina hayo ambayo yatapigiwa kura kwa kuzingatia kiwango cha mchezaji na nidhamu kwa jumla.

“Kama ulivyo utaratibu wa Azam FC, jopo la viongozi wamepitisha majina matatu ya wachezaji akiwemo Sure Boy, Mbaraka na kipa Razark kwa ajili ya kuchuana katika tuzo ya Septemba ambapo mashabiki wa soka ndiyo watakaopata nafasi ya kupiga kura kupitia mitandao ya kijamii na atakayepata kura nyingi ndiyo atakayeibuka mshindi.

“Vigezo vitakavyozingatiwa ni nidhamu ya mchezaji, uwezo wa kujituma uwanjani na vitu vingine, vitu vyote hivyo vitaamuliwa na mashabiki kama ilivyo mwezi uliopita tulipompata mchezaji bora wa mwezi wa nane ambaye alikuwa Yakub Mohamed, hivyo tunawaomba wadau kufuatilia mechi zetu za Azam kisha kupiga kura na si kubuni,” alisema Jaffari.

Aidha, wachezaji hao walipoulizwa kuhusiana na tuzo hiyo walieleza kuwa, wamefurahishwa na hatua hiyo iliyochukuliwa na viongozi wao huku kila mmoja akiahidi kuitwaa tuzo hiyo na kudai kuwa itawaongezea morali ya kujituma zaidi katika kila mechi. 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic