Kikosi cha Simba kinatarajia kuwasili nchini kesho alfajiri kikitokea nchini Djibouti.
Simba iliitwanga Gendamarie kwa bao 1-0 katika mechi ya Kombe la Shirikisho na kufanikiwa kufuzu kwa jumla ya mabao 5-0.
Kikosi hicho kitatua nchini kesho saa 7 usiku (baada ya leo saa 6 usiku) kikitokea Djibouti kupitia Nairobi.
Simba inarejea nchini kuendelea na maandalizi ya michezo yake ya Ligi Kuu Bara huku ikiwa inajiandaa kucheza dhidi ya Waarabu wa Misri, Al Masry.
0 COMMENTS:
Post a Comment