July 26, 2018


Na George Mganga

Uongozi wa klabu ya Coastal Union ya Tanga umethibitisha kuingia mkataba na Nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Saleh Kiba maarufu kama King Kiba.

Coastal wamefikia maamuzi ya kumsainisha Kiba kwa kile walichokieleza kuwa ana kipaji cha mpira na wanaamini ataisaidia klabu hiyo.

Klabu hiyo imesema tayari jina la Kiba limeshawekwa kwenye mfumo wa mpya wa usajili unaotumika hivi sasa (TFF FIFA CONNECT) ambapo dirisha la usajili litafungwa leo majira ya saa 6 kamili usiku.

Taarifa za awali kutoka uongozi wa Coastal zilizema kuwa Kiba alikwenda mwenyewe kuomba nafasi ya kuichezea klabu hiyo kutokana na mapenzi yake ya kucheza mpira wa miguu.

Baada ya kuomba nafasi hiyo, uongozi wa Coastal Union ulianza mazungumzo ya kumalizana na Kiba na sasa atakuwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo msimu ujao.






1 COMMENTS:

  1. Ali Kiba ataipaisha sana Coastal Union..!
    Promo la kutosha hilo..!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic