MSHAMBULIAJI wa Stand United, Alex Kitenge amedai hali ngumu ya uchumi inayoikumba klabu hiyo inamfanya afikirie kurudi kwao Burundi ili akaangalie maisha mapya ya soka. Mshambuliaji huyo amekiri kwamba Stand inapitia mazingira
magumu kiuchumi.
“Ni miezi minne imepita sijapata mshahara wangu na wala sielewi nitapewa lini, nimejaribu kuongea na uongozi wamesema watanipa mshahara wangu ili niendelee kuitumikia klabu hii, tofauti na hapo mimi naondoka kwetu ili nikajipange upya na kuangalia timu nyingine ambayo inaweza kunilipa kulingana na huduma ninayoipa timu husika,” alisema Kitenge ingawa viongozi wake wamekwepa kuzungumzia hali inayoendelea ndani ya timu hiyo.
Stand United itacheza na Wekundu wa Msimbazi, Simba Jumapili, Taifa. Stand ni miongoni mwa timu za Ligi Kuu Bara ambazo zinahaha kikubwa ikielezwa kwamba ni kukosekana kwa mdhamini mkuu wa Ligi Kuu Bara inayoendelea
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kama St. Aug. Tu.
ReplyDelete