SERIKALI kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na
Michezo, Harrison Mwakyembe imeahidi msaada wowote kwa Kocha wa Taifa Stars,
Emmanuel Amunike kuhakikisha timu hiyo inafuzu Afcon.
Mwakyembe amesema kuwa;
“Nimefurahishwa sana na matokeo haya , vijana wamenikuna uwezo waliouonyesha ni
mzuri, sisi kama serikali tutakuwa tayari kumsapoti mwalimu kwa chochote anachokihitaji ili kuweza kufanikisha kucheza
Afcon.”
“Tumefurahishwa lakini tusiwe na miluzi mingi, masuala ya kiufundi
tunamuachia mwalimu aweze kufanikisha malengo.
“Pia nimefurahishwa na muitikio
wa mashabiki uwanjani kushangilia, huu ndio uzalendo unaotakiwa, tutumie njia
hii kuwamaliza Uganda wakija hapa nyumbani, nawapongeza sana,” alisema
Mwakyembe akiizungumzia Stars ambayo ikishinda mechi ijayo dhidi ya Lesotho
inafuzu kama Uganda akimpiga Cape Verde.
0 COMMENTS:
Post a Comment