December 30, 2018


Kuelekea kikao cha wachezaji wa zamani na Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, hapo kesho, imeelezwa kocha huyo hahitaji majadala wowote kuhusiana na Beno Kakolanya.

Zahera alikubali wito wa wachezaji hao ambao wana lengo la kuzungumzia masuala mbalimbali ya soka ambapo kesho watakuna katika makao makuu ya klabu hiyo.

Taarifa imesema Zahera amekubali kwa moyo mmoja lakini hataki kusikia akigusiwa suala la Kakolanya ambaye alisema hahitaji kumuona tena kwenye kikosi chake.

Kocha huyo mwenye mikwara mizito, amefunguka kuwa anaweza akashindwa kuwasikiliza wachezaji hao wakianza kumzunguzia Kakolanya kwani aligomea mazoezi kisa fedha.

Taarifa imeongeza kuwa Zahera anataka wajadili mambo mbalimbali ikiwemo ya usajili na namna ya kuisaidia Yanga haswa kifedha kutokana na hali inayopitia hivi sasa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic