BONDIA Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ ameweka wazi kwamba hivi karibuni anatarajia kupambana pambano la Ubingwa wa Dunia kwa kuzichapa na bondia kutoka nchi za Uingereza au Hungary.
Mbabe amesema kwamba pambano hilo litakuwa mwezi Machi mwaka huu, huku kwa sasa menejimenti yake ndiyo inahangaikia kuratibu pambano hilo.
“Mwezi wa tatu nitapanda ulingoni kwa ajili ya kuzichapa na bondia ambaye anaweza kutoka Uingereza au Hungary, ambapo menejimenti yangu ndiyo ambayo inasimamia kila kitu, mimi ninasubiri kupambana tu,” alisema Mbabe.
0 COMMENTS:
Post a Comment