Dakika 83 zilitosha kuonesha makali ya kisu cha wana Jangwani kwenye uwanja wa Majaliwa uliopo Ruangwa mkoani Lindi baada ya Deus Kaseke kumimina krosi maridadi iliyomkuta Heritier Makambo katika eneo sahihi na kumalizia kichwa kilichozama wavuni.
Mlinda mlango wa Namungo FC ambaye dakika zote 83 alikuwa nyota wa mchezo aliishiwa nguvu baada ya kushtuka mpira upo kambani, licha ya jitihada za Namungo kutafuta sare walikuwa wamechelewa kwani safu ya ulizi ya Yanga haikuruhusu kuchinjwa ugenini.
Matokeo hayo yanaifanya Yanga isonge mbele hatua ya nane bora ikisubiri mpinzani wake ambaye watakutana naye baada ya droo kuchezwa hivi karibuni.
0 COMMENTS:
Post a Comment