MKURUGENZI Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo usiku wa jana alikuwa miongoni mwa waliokabidhi tuzo za Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival, (SZIFF 2019).
Tuzo hizo zilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City, Februari 23,2019 ambapo Shigongo alitoa tuzo katika Kipengele cha Muigizaji Bora wa Kike katika World Cinema ambapo walitangazwa washindi wawili, Leena Alam kutoka Afghanstan na Myra Vishwakarma kutoka India.
Hii ni mara ya kwanza kwa Shigongo kufanya hivyo hali inayomfanya aweke historia hizo za tuzo ambazo zilihudhuriwa na watu mashuri na wanasiasia kama Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe.
0 COMMENTS:
Post a Comment