HIZI hapa zimefanikiwa kupenya hatua ya 16 bora kwenye kombe la Shirikisho na kutinga hatua ya robo fainali:-
Singida United kutoka mkoani Singida iliifungashia virago Coastal Union ya Tanga kwa bao 1-0 mchezo uliochezwa Uwanja wa Chamazi.
Kagera Sugar iliyo chini ya Mecky Maxime iliifungashia virago timu ya Boma kwa kuifunga mabao 2-1.
KMC ya Dar es Saalaam iliwaondoa mabingwa watetezi Mtibwa Sugar baada ya dakika 90 kukamilika kwa sare ya kufungana bao 1-1 ilishinda kwa penalti 4-3 Uwanja wa Chamazi.
Lipuli ya matola ilishinda dhidi ya Dodoma ya Julio kwa mabao2-1.
Yanga imeichinja Namungo FC kwa bao 1 la usiku Uwanja wa Majaliwa.
Alliance FC ya Mwanza imeitungua Dar City ya Tanga mabao 3-0.
African Lyon ya Dar imeitungua Mbeya City ya Mbeya kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya dakika 90 kukamilika kwa sare ya mabao 2-2 Uwanja wa Uhuru,
Bingwa wa msimu huu atakuwa ni mpya kutokana na kuondoshwa kwa bingwa mtetezi Mtibwa Sugar.
0 COMMENTS:
Post a Comment