Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kunoa timu ya mabingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.
Hatua hiyo ni baada ya kufikia malengo aliyowekewa katika mkataba unaomalizika hivi karibuni kwa kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara kufika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Taarifa iliyotolewa leo kupitia mitandao ya kijamii ya Simba haijaweka bayana malengo mapya ambayo kocha huyo amepewa.
Ni muda muafaka kutengeneza timu ya kushindana Kimataifa ambayo haitakamatika Tanzania.
ReplyDelete