Katika kuhakikisha inazidi kuwafurahisha wateja wake, Kampuni ya
Michezo ya Kubashiri Tanzania, SportPesa Tanzania leo imezindua promosheni mpya
inayofahamika kama ‘USIBAHATISHE CHEZA NA SPORTPESA’.
Promosheni
hiyo itakuwa ya kushindania gari ndogo tatu (3) aina ya IST, Simu janja za
kisasa Smartphone 200, tiketi 45 za mechi ya Simba dhidi ya Sevilla FC
inayoshiriki Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) na tiketi 10 za mchezo wa
Kariobangi Sharks na Everton ya England utakaochezwa nchini Kenya.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa Tanzania,
Tarimba Abbas amesema wamezindua promosheni hiyo ambayo imeanza toka Mei Mosi
na itakuwa kwa wiki 15, kwa malengo ya kampuni kuzidi kuwa karibu na wateja
wake.
“Tumezindua
promosheni mpya inayokwenda kwa jina la ‘Usibahatishe Cheza na SportPesa’,
ambayo tutatoa magari matatu (3) ya kisasa kabisa aina ya IST.
“Lakini
tutatoa zawadi ya simu za kisasa pia Smartphone 200 ambazo zitaenda kwa wateja
wetu watakaoshinda katika droo tutakazochezesha,” anasema na Tarimba na
kuongeza.
“Pia, tutatoa
tiketi 45 za mechi ya Simba ambayo itacheza na mabingwa wa Hispania (La Liga),
timu ya Sevilla ambao watacheza tarehe 23 mwezi huu kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam. Lakini tutatoa tiketi zingine 10 za kwenda kuangalia
mechi ya timu ya Kariobangi Sharks watakaocheza na Everton ya England
watakaocheza nao kule Kenya.
“Promosheni
hii itachezeshwa kwa droo 15 kwa wiki 15 kwa kuwapata washindi. Hivyo kila siku
ukibeti unashinda zawadi, sasa huu ni wakati wa Watanzania kuchangamia fursa
hiyo,” anasema.
Tarimba,
anasema kuwa leo wameanza kwa kutoa simu za Smartphone sita (6) na tiketi za
mechi ya Simba dhidi ya Sevilla 13, baada ya kuibuka washindi wa droo ya
kwanza.
“Tunajisikia
faraja kurudisha fadhila kwa Watanzania, hasa wateja wetu, sasa huu ni wakati
wao kucheza zaidi na SportPesa ili kujishindia zawadi zetu hizi mpya za gari,
simu na tiketi za mechi hii kubwa ya Simba na Sevilla,” anasema.
Sevilla inatarajia kuwasili nchini Mei 21,
kisha kucheza na Simba Mei 23 mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, kufuatia mwaliko wa kampuni ya michezo ya kubahatisha nchini, SportPesa
Tanzania.








0 COMMENTS:
Post a Comment