July 11, 2019




Abdulhalim Humud aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa timu ya KMC kwa sasa yupo kwenye mchakato wa mwisho kukamilisha dili yake kutimkia Uarabuni kwa ajili ya kupiga soka la kulipwa.

Habari kutoka kwa mtu wa karibu zimeeleza kuwa Humud anakamilisha taratibu za mwisho kutimkia kwenye Falme za Kiarabu kwenda kusakakata soka.

“Mpango wake mkubwa kwa sasa ni kuondoka Bongo kutokana na mikasa ambayo amekuwa akipitia ili kujiweka mbali, ila ameshapata timu moja iliyopo kwenye Falme za Kiarabu,"kilieleza chanzo.

Humud amesema kuwa mipango ya kuondoka ama kubaki itakuwa wazi endapo mipango itakamilika kwani kwa sasa anakamilisha taratibu za mwisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic