TAYARI muda
unazidi kukimbia kwa kasi ambayo haiwezi kuzuilika hivyo ni muda mwafaka kwa
kila timu kuanza kujipanga kwa ajili ya msimu unaofuata.
Kwa sasa ni
usajili tu ndio umepamba moto hili haliepukiki ni lazima kila timu ifanye
usajili kwa kuboresha kikosi na kukifanya kiwe cha ushindani msimu ujao.
Ambao bado
hawajaanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msimu ujao hata kwa kuaandaa mipango
kazi wanajiweka kwenye mazingira magumu ligi ikianza.
Viongozi wa
timu pamoja na benchi la ufundi ni muda wa kukaa na kufanya mipango makini kwa
ajili ya msimu mpya unaofuata.
Wengi
wanajisahaulisha baada ya ligi kuisha wanadhani wamemaliza kila kitu kumbe kuna
mambo ambayo yanapaswa yafanyiwe kazi.
Kuangalia
mapungufu ambayo msimu uliopita yalisumbua na kuanza kuyafanyia kazi ni vitu
vya muhimu kwa muda huu kabla ligi haijaanza.
Kufanya
maandalizi ya awali na kukaa na timu ni jambo ambalo haliwezi kuepukika hasa
ukizingatia kwamba wengi wanafanya usajili.
Muda wa
maandalizi ya awali utakuwa muda wakuwafanya wachezaji wawe kitu kimoja na
benchi la ufundi kutambua aina ya kikosi walichonacho.
Pia wale
ambao wanapuzia kufanya maandalizi ya awali ni muda wao kushtuka kwamba kama
hawatafanya wakati huu wakati ujao watavuna kile walichokipanda.
Isiwe
maandalizi yapo kwenye timu ambazo zinashiriki Ligi Kuu Bara pekee bali iwe na
kwa zile ambazo zinashiriki Ligi Daraja la Kwanza nazo ni lazima zifanye
maandalizi.
Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) mipango yao iwe wazi na itazame makosa ambayo yalitokea
msimu uliomalizika kwa sasa yasijirudie.
Kwa
kuwakumbusha tu kama watakuwa wamesahau suala kubwa la viporo kwa msimu
uliopita lilivuruga na kuua kabisa utamu wa ligi.
Ilifika
wakati timu zimemaliza mzunguko wa kwanza nyingine bado zilikuwa hazijacheza
mechi nyingi hii ilikuwa inavuruga na kuua kabisa ushindani wa ligi.
Hapa kuna
jambo la msingi ambalo linatakiwa kufanyika hasa msimu mpya ambao unatarajiwa
kuanza Agosti 23.
Ratiba
iliyopangwa na kuwekwa wazi na Bodi ya Ligi Tanzania ni lazima ifuatwe na
izingatie kanuni ambazo zimewekwa.
Kwa kufanya
hivyo kutafanya ligi iwe bora na yenye ushindani hali itakayoongeza mvuto wa
ligi msimu mpya.
Ligi
isivurugwe bali ipewe thamani kubwa itakayofanya kila mmoja apende kuitazama na
kuifuatilia bila kujali timu gani inacheza.
Kwa upande
mwingine suala la viwanja limekuwa tatizo kubwa hasa kwa timu nyingi kutokuwa
na viwanja vyao vya kudumu.
Viwanja
vingi ambavyo msimu ulipota vilitumika viwango vilikuwa vya chini jambo
lililofanya matokeo kuwa ya shida kupatikana kutokana na ubora wa viwanja.
Mfano
ukitazama hali halisi ya viwanja vyenye ubora bado ni vichache sana na
vinahesabika tofauti na idadi za timu ambazo zipo.
Vuta picha
uwanja wa Mkwakwani ambao unatumika na timu ya Coastal Union ya Tanga namna
ulivyo timu inacheza kwenye mazingira magumu.
Pia ukienda
Namfua pale Singida ni shida kupata matokeo chanya kwa timu ambayo haijauzoea
uwanja na hata wenyeji wakati mwingine wamekuwa na taabu kupata matokeo.
Ni muhimu
kwa TFF kuweka masharti magumu kwa kila timu ambazo zinashiriki ligi kuwa na
viwanja bora na kuvikagua kabla ya ligi kuanza ili kuepusha sababu ambazo
zinaweza kuepukika.
Bora kuwa na
viwanja vichache ambavyo vinakidhi viwango kuliko kuwa na viwanja vingi ambavyo
havikidhi viwango kwa ajili ya kuchezea.
Uwanja kama
ule wa Samora upo vizuri na unaleta raha kwa timu kucheza michezo yao pale
kwani ni sehemu bora na inapendeza.
Ukigusa na
Azam Compex nao pia wamewekeza na wanapaswa kuwa mfano kwa timu zote hapa Bongo
hasa kwa uwekezaji na namna ambavyo wanaendesha timu zao.
Napenda
kutoa rai kwa TFF msimu huu waongeze zaidi umakini na kufanya kazi kwa weledi
ili kuiboresha ligi yetu iwe na msisimko tofauti na muda mwingine.








Hivi unaanzaje kuwashauri au kuwakosoa TFF japokuwa wana mapungufu wakati wewe mwenyewe na timu yako ya waandishi wa blog ni majanga.Nakushauri kabla hujawanyooshea kidole TFF ungeanza wewe kurekebisha mapungufu makubwa katika uandishi wenu wa habari usio na mwelekeo na wenye kukera wengi.Habari nyingi ni za kupika kiasi kwamba inafikia vichwa vya habari na habari yenyewe ni tofauti kabisa na ukisoma kwa makini unagundua ni habari za kutunga.ANZA WEWE KWANZA KUJIREKEBISHA ILI TUKUUNGE MKONO UNAPOKOSOA WENGINE...
ReplyDeleteUnawashauri nini hao tff wapo hapo kwa maslahi yao na kujaza matumbo yao tu viporo vingi vilifanywa kwa malengo maalum na wewe mwandishi unalielewa hilo sasa hivi unajifanya msahuri kwa jinsi unavyojitoa fahamu na nyinyi tff ni wakati wa kukaa pembeni mshathibitisha mmefeli kabisa tena wala hamna weledi wa uongozi wa mpira na huyo Wambura wenu hamana kitu kabisa debe tupu kwa ufupi muondoke msingoje aibu,mmeshindwa hata kwenda kwenye mkutano na Waziri wa michezo.
ReplyDelete