KWASI ANUKIA TIMU NYINGINE LIGI KUU
Kama mlidhani Asante Kwasi amechuja, ngoja ishu yake na Biashara itiki asaini mkataba wa Kocha Amri Said.
Kwasi ni kati ya wachezaji ambao mikataba yao ilimalizika ya kuichezea Simba.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo limezipata gazeti la Spoti Xtra kutoka Global Publishers, Kwasi yuko kwenye hatua nzuri na Biashara United.
“Uongozi umepania kukifanyia marekebisho kikosi chake na katika hilo umepanga kuwasajili wachezaji wenye uzoefu wa kucheza mechi za ligi na kati ya wachezaji hao yupo Kwasi,” alisema mtoa taarifa ndani ya uongozi wa Biashara.








Ulishauriwa mapema kusaini Yanga kwa sababu kule ulipochagua ulikuwa huna nafasi lakini ukapuuzia ulichokipata ni hicho kwenda katika timu inayopambana isishuke daraja
ReplyDelete@Salehjembe mkataba wa Kwasi na Simba unaisha December kwani kwasi alisajiliwa kwa misimu miwili na alisajiliwa baada ya kuidungua Simba raundi ya kwanza dhidi ya Lipuli. Hivyo si kweli unavyosema mkataba wa Kwasi na Simba uliisha. Simba inabidi wamlipe kwa kuvunja mkataba.
ReplyDelete