DIRISHA la
usajili linaendelea kwa sasa ambapo timu nyingi zinajipanga kwa ajili ya msimu
mpya wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza Agosti 23.
Kuna umuhimu
mkubwa kwa kila timu kuanza maandalizi mapema kwani matokeo chanya uwanjani
yanatengenezwa na maandalizi ya awali ambayo timu huwa zinafanya.
Muda wa
kufanya haya yote ni sasa kwa kuanza na usajili makini pamoja na kambi bora
zitakazofanya kila timu kupambana kikamilifu msimu ujao.
Kwa timu
zote bila kujali zinashiriki Ligi Kuu Bara ama Ligi Daraja la kwanza ni muhimu
kujipanga vema.
Wale ambao
wamekuwa wakifanya usajili kwa mapezi yao ama kutumia nafasi zao za uongozi si
sawa kwani anayejua uhitaji wa wachezaji ni kocha mwenyewe.
Itapendeza
endapo viongozi watafuata ripoti ya kocha kwenye kufanya usajil jambo liakaloepusha
lawama na malalamiko kwa benchi la ufundi kwani wao ndio wanahusika kwenye
suala la kupanga timu.
Kwa kupitia
yale mapungufu ambayo benchi la ufundi limeyaona hapo ndipo kazi inabidi ifanyike
na sio kusajili kwa kufuata mkumbo.
Kila mmoja
amekuwa ana mamlaka hasa linapofika suala la usajili kulingana na mapenzi
ambayo anayo kwa mchezaji ama wengine ni wale ambao wanaona kwamba watapata
faida endapo watamsajili mchezaji fulani.
Sasa suala
la kutazama faida huwa linakuwa kwa muda tu tofauti na yule ambaye atasajili
kwa kufuata mapendekezo ya mwalimu itasaidia kujenga kikosi imara.
Ikumbukwe
kuwa wakati timu ikiboronga anayepewa mzigo wa lawama siku zote huwa ni mwalimu
hivyo itakuwa vizuri endapo ripoti itafanya kazi lawama zitakuwa haziepukiki
kwake.
Naona timu
nyingi zinapambana kutafuta wachezaji ambao wanaona kwamba wanawafaa kwenye
kikosi chao kwa ajili ya kuleta ushindani msimu ujao.
Tukiachana
na suala la usajili wa ligi ambao unaendelea kwa sasa ngoja tuzungumzie pia
suala la maandalizi ya michuano ya CHAN ambayo inatarajiwa kufanyika hivi
karibuni.
Muda mzuri
kwa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) kuanza maandalizi mapema kwa ajili ya
timu yetu ya Taifa ili ifanye vema na kuwatoa kimasomaso mashabiki.
Ikumbukwe
kwamba timu imefanya vibaya kwenye michuano ya Afcon ambayo inaendelea nchini
Misri huku timu yetu ya Taifa ikitolewa kwenye hatua za awali.
Kwa sasa
itakuwa vema wachezaji wakitumia michuano hii kufanya ushindani wa kweli na
kupata matokeo chanya kwenye michuano ambayo inatajia Kuanza hivi karibuni.
Kama
wachezaji watatumia vema michuano hii ya CHAN itarudisha ile imani ambayo
ilikuwa imeanza kupotea kwa mashabiki na kuwafanya wawe kitu kimoja.
Mashabiki
wanapenda mpira hii ipo wazi na haiwezi kufichika kwani ukirudisha kumbukumbu
kwenye mchezo wa mwisho ambao ulichezwa uwanja wa Taifa mashabiki walionyesha
mapenzi yao wakati timu ilipocheza na Uganda.
Wachezaji
wanapaswa watambue kwamba wana kazi ya kufanya kurejesha imani kwa mashabiki na
kazi yao ni moja tu kupata matokeo chanya.
Maandalizi
mazuri kwa timu ya Taifa yanapaswa yaanze kufanyika sasa kabla ya kuanza
kujutia hapo baadaye ikitokea tukaboronga tena.
Kila kitu
kwenye soka kinawezekana na ipo wazi kwa muda huu malipo ya wachezaji yawe wazi
na wajitoe kwa moyo mmoja kufanya kazi na kutafuta matokeo.
Benchi la
ufundi litazame namna bora ya kufanya kuongoza kikosi kiwe na ushindani na
morali bora kwenye michuano hii ya ndani.
Nidhamu inapaswa
ipewe kipaumbele na wachezaji waingie kazini kwa juhudi kubwa bila kutafuta
matokeo wakiwa ndani ya uwanja.
Mashabiki
pia tusiwe nyuma katika hili kazi ya kutoa sapoti ni muhimu kwani uwepo wa
mashabiki unaongeza morali na hamasa kwa wachezaji wakiwa uwanjani.
Bado tuna
imani na timu yetu hasa ukizingatia kwamba wachezaji wengi wameanza kutambua
thamani ya kucheza ndani ya timu ya Taifa.
Wale
watakaochaguliwa kuitumikia timu ya Taifa wafanye kazi kwa moyo kupeperusha
Bendera ya Taifa kwani watakuwa wameaminiwa kiasi kikubwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment