August 22, 2019


Na George Mganga,
Dar es Salaam

Uongozi wa Simba kupitia Ofisa Habari wake, Haji Manara, umesema utalipia gharama za kikao na waandishi wa habari ambacho wamedhamiria kukifanya kitakachohusisha wasema wa klabu zote zinazoshiriki mashindano ya kimataifa.

Tanzania Bara inawakilishwa na timu nne kunako michuano ya kimataifa ambazo ni Simba SC pamoja na Yanga zinazoshiriki Ligi ya Mabingwa huku Azam FC na KMC FC zikishiriki Kombe la Shirikisho Africa.

Katika kikao na waandishi wa habari juzi, Manara alisema kuwa watafanya kikao hicho kwa ajili ya kuungana pamoja kuonesha utaifa sababu wote wanaiwakilisha nchi.

Alieleza kuwa wao kama Simba watahusika kugharamikia kikao hicho kwa kuwa wana uwezo wa kufanya hivyo.

"Tumepanga kufanya kikao cha pamoja na wasemaji wa timu zote zinazoshiriki mashindano ya kimataifa.

"Lengo letu kubwa ni kuonesha kwanza utaifa kwa kuwa tunaiwakilisha nchi, hakuna sababu ya kutofautiana, lazima tupeane sapoti.

"Sisi kama Simba tutagharamikia kikao hicho, hilo halitakuwa na shida sisi kwetu kama mabingwa wa nchi," alisema Manara.


13 COMMENTS:

  1. Hongera sana manara na huwo ndo uzalendo

    ReplyDelete
  2. Manara sijakusoma vizuri! Try again.

    ReplyDelete
  3. dharau kwani ameambiwa yanga hawana uwezo wa kulpia acha dharau ww ucyejtambua kkao umektaka ww sasa maneno hayo ya kejeli ya nn?

    ReplyDelete
  4. Hawa jamaa wamekuwa watete Sana wanayo Ile inayoitwa inferiority complex wanahisi wao kama vile wanaonekana wa hali ya chini masikini na kuona wanadharauliwa na hata wakitajiwa kuzuri wao wanakiona kibaya

    ReplyDelete
  5. Uhamasishaji wa Manara Ni wa hali ya juu wakusisimuwa na kutisha. Mungu kampa kipaje

    ReplyDelete
  6. Najua Yanga hawatakuja

    ReplyDelete
  7. Hicho kikao Yanga wakikiudhuria watakuwa wamejidhalilisha kwani Manara siyo msemaji wao na pia si anayepanga ratiba yao. Hata hivyo Manara siyo msemaji wa Simba bali ni Mhamasishaji wa Simba hivyo amwombe msemaji wa Simba akutane na wa Yanga wapange jinsi ya kukutana na Yanga watakuwa tayari kulipia kikao hicho.

    ReplyDelete
  8. Hicho kikao kinachotaka kupangwa wala hakikuja wakati mwafaka,kwanin wasingefanya kabla ya game za kwanza wakati Yanga yuko nyumbani?wanasubir wao mechi zao za nyumbani ndio waweke hamasa,hio wala haitokuwa msaada kwa yanga,maana ya kikao ni kuhamasisha pia washabiki kujitokez kwa wingi uwanjan na kushangilia timu zetu za tanzania,wakati timu moja kati ya hizo ipo ugenini,,

    ReplyDelete
  9. Haji is the big Brand.Elimisha vyura sports the way to support the gamez

    ReplyDelete
    Replies
    1. This comment has been removed by the author.

      Delete
  10. Angekuwa mzalendo angefanya hilo wakati yanga inacheza hapa sio amesubiria simba inakuja kicheza home ndio anajinadi mzalendo.Wazo zuri ila atalifanya kwa maslahi ya timu Fulani.Kingefanyika wakati timu zote hazijaanza mechi za kimataifa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic