MOTO wa Ligi
ya Mabingwa Afrika pamoja na ule wa Kombe la Shirikisho umeanza kuwaka kwenye
viwanja tofauti ambapo wawakilishi wetu wanapambana kupeperusha Bendera ya
Taifa.
Tanzania
imepata fursa ya kuwa na timu sita ambazo zinapeperusha Bendera kimataifa hivyo
ni fursa nzuri kwa wachezaji pamoja na timu kuandaa mambo mazuri kwa ajili ya
mashabiki wao.
Tumeona Timu
ya Taifa ya Wanawake ‘Tanzanite’ wametwaa Kombe la COSAFA, wanastahili pongezi
kwa hilo.
Hii inamaanisha
kwamba kila kitu kikipangwa kinawezekana kutokea vile ambavyo tunafikiria, uwe
mwanzo na mwendelezo kwenye michuano mingine.
Kwa upande
wa Tanzania kuna Simba, Yanga ambazo hizi zipo upande wa michuano ya Ligi ya
Mabingwa Afrika huku Azam FC na KMC wao wakipeperusha Bendera kwa upande wa
Kombe la Shirikisho Afrika.
Visiwani
Zanzibar ni KMKM ambao hawa wanawakilisha nchi kwenye michuano ya Ligi ya
Mabingwa Afrika na Malindi kwa upande wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Tumeona
mechi za mwanzo timu zote zimeonyesha jitihada ya kupambana kusaka matokeo
ambapo Simba, KMC, na Malindi walikuwa ugenini na wamelazimisha sare ya bila
kufungana.
Simba wao
walikuwa nchini Msumbiji walimenyana na UD Songo ya Msumbiji, KMC ilikuwa
Rwanda ilimenyana na AS Kigali huku Malindi ya Zanzibar ilikuwa Somalia
ikicheza na Mogadishu City.
Hili ni
fungu la kwanza ambalo kazi yake sio ya mchezo kwani wengi wanajipa nafasi ya
kupata matokeo na kusahau kwamba kwenye mpira kila timu inatafuta matokeo
chanya.
Kwa sare
walizopata hawa wawakilishi wetu kimataifa kazi yao kubwa ni kupanga mikakati imara
na sio kujipa matumaini kwamba watapenya wasipojipanga wataangukia pua.
Mechi za
marudio zitakuwa nyumbani hivyo kazi yao kubwa ni kutumia vema fursa ambayo
wapinzani wao wameshindwa kutumia mwanzo kwani kwa sasa kila timu inapambana
kupata matokeo.
KMKM
ina kumbukumbu ya kupoteza kwa kufungwa mabao 2-0 na de Agosto ya Angola wana kazi ya kwenda
kupindua meza ugenini na inawezekana kukiwa na nia ya kutafuta ushindi.
Kwa upande
wa Azam FC ambao walipoteza mbele ya Fasil Kenema naona bado ina nafasi ya
kupenya hatua hii ya awali ya michuano ya kombe la Shirikisho.
Watanzania
katika hili tunatakiwa kuungana na kuzipa matumaini timu zetu kuelekea kwenye
michezo ya marudio ili wapate matokeo, Azam wanautambua vema uwanja wao wa
Chamazi kazi yao itakuwa moja tu kuwafunga wapinzani wao.
Naona wengi
kama wameanza kuipotezea ramani Yanga na kuipa kiburi Simba kwamba itapata
matokeo hakuna wepesi katika michuano ya kimataifa hasa kwenye mechi za awali.
Hivyo nina amini
Yanga inakwenda kufanya kitu cha kipekee kwenye mchezo wa marudio dhidi ya
Townshp Rollers ya Botswana na wengi hawataamini.
Kitu pekee
ambacho Kocha Mkuu, Mwinyi Zahera anapaswa kukifanya kwa sasa ni kurekebisha
makosa madogo ambayo yameonekana kwenye mchezo wa kwanza.
Kwa namna
ambavyo wachezaji wamecheza mchezo wa kwanza kuna kitu ambacho kimejificha hasa
kiuwezo hicho ndicho ambacho kinapaswa kitumike mchezo wa marudio.
Kuruhusu
kufungwa kwenye michuano ya kimataifa hatua ya awali sio matokeo mazuri ila kwa
kuwa nao wamefunga bao basi safu ya ushambuliaji ina mzigo wa kufanya vema
mchezo wa marudio.
Safu ya
ulinzi inatakiwa iongeze umakini na kufanya maboresho madogo ambayo walikuwa
wameshindwa kuyafanya wakati walipocheza Uwanja wa Taifa.
Imani yangu
ni kwamba ukubwa wa Taifa na michuano ilivyo kila timu ina nafasi ya kupenya
jumla endapo itapambana na mikakati ikiwa makini.
Zile ambazo
zinajipa nafasi ya kushinda zinapaswa ziwe makini zisijiamini kupita kiasi
zitapoteana uwanjani na habari yao itaishia hapo, mpira ni mchezo unaohitaji
nidhamu na umakini.
Mashabiki
kwa michezo ambayo itakuwa nyumbani ni wajibu kujitokeza kuzisapoti timu zetu
zikiwa uwanjani kuzipa sapoti.
0 COMMENTS:
Post a Comment