September 3, 2019


Kamati ya Bodi ya Ligi Kuu ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake cha Septemba 2, 2019 ilipitia matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2019/2020 iliyoanza rasmi Agosti 24, 2019 na kufanya uamuzi ufatao;

Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera ametozwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kuvaa mavazi yasiyo nadhifu na ya heshima katika mechi hiyo, kinyume na Kanuni ya 14(2m) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Adhabu dhidi yake imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 41(13) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.

•Klabu ya Yanga imepewa Onyo Kali kwa kushindwa kuhakikisha Kocha wake Mwinyi Zahera anaongoza benchi la ufundi la timu yake akiwa katika mavazi nadhifu na ya heshima.

Adhabu dhidi ya klabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

9 COMMENTS:

  1. Vita dhidi ya Yanga si ndogo....sasa tusubiri reaction ya wapenzi wa soka wa timu ya wananchi ....vurugu yake si haba ....itajengengeka dhana kuwa sheria na kanuni ziliundwa zikiwa na kusudio kwa mlengwa wa adhabu....Kuongoza Soka kwa chuki si "afya" kwa maendeleo ya mpira wa Tanzania....Yanga msitoke nje ya reli jiandaeni na Zesco mashabiki waujaze uwanja wa Taifa

    ReplyDelete
  2. Zahera alikuwa akihisi kuwa yeye yupo juu ya kanuni na yupo huru kufanya au kusema anachotaka yeye mwenyewe bila ya kuingiliwa na yeyote

    ReplyDelete
  3. Vita dhidi ya Yanga si ndogo....sasa tusubiri reaction ya wapenzi wa soka wa timu ya wananchi ....vurugu yake si haba ....itajengengeka dhana kuwa sheria na kanuni ziliundwa zikiwa na kusudio kwa mlengwa wa adhabu....Kuongoza Soka kwa chuki si "afya" kwa maendeleo ya mpira wa Tanzania....mapungufu ya kiutendaji na kiutawala yanapoainishwa na kusemwa inakuwa makosa....uhuru wa kukosoa na kutoa maoni ni uhuru wa kikatiba ambao kila mtu anao uhuru huu usikandamizwe kwa kutunga kanuni na sheria...ili kuzuia watu kukosoa mapungufu yanayotokea katika uendeshaji na usimamizi wa tasnia ya mchezo wa soka hapa Tanzania.

    USHAURI
    Yanga msitoke nje ya reli jiandaeni na Zesco mashabiki waujaze uwanja wa Taifa..ili muudhihirishie umma Yanga ni baba lao

    Ahsante

    ReplyDelete
  4. Angekuwa mzungu wasingemgusa Ila mswahili mwenzetu ndo hivyo tena. Mavazi nadhifu ndo yapi hayo?

    ReplyDelete
  5. Replies
    1. Vita dhidi ya Yanga si ndogo....sasa tusubiri reaction ya wapenzi wa soka wa timu ya wananchi ....vurugu yake si haba ....itajengeka dhana kuwa sheria na kanuni ziliundwa zikiwa na kusudio kwa mlengwa wa adhabu....Kuongoza Soka kwa chuki si "afya" kwa maendeleo ya mpira wa Tanzania....mapungufu ya kiutendaji na kiutawala yanapoainishwa na kusemwa inakuwa makosa....uhuru wa kukosoa na kutoa maoni ni uhuru wa kikatiba ambao kila mtu anao uhuru huu usikandamizwe kwa kutunga kanuni na sheria...ili kuzuia watu kukosoa mapungufu yanayotokea katika uendeshaji na usimamizi wa tasnia ya mchezo wa soka hapa Tanzania.

      USHAURI
      Yanga msitoke nje ya reli jiandaeni na Zesco mashabiki waujaze uwanja wa Taifa..ili muudhihirishie umma Yanga ni baba lao

      Ahsante

      Delete
  6. Kama kweli mnapenda maendeleo ya soka letu shughulikieni pia changamoto zinazotolewa na makocha wa club zetu, wao ni wataalam wa soka, heshimuni taaluma zao. Kuna malalamiko mengine yanakuwa na mashiko. Ili tuwe na timu ya taifa iliyo bora tunahitaji kuwa na kanuni bora za kuliendesha soka letu. Adhabu sawa, lkn je kero za msingi ziendelee kupigiwa kelele kila kukicha, hamuoni umuhimu kuwa soka linapaswa kuongozwa kisayansi pia? Kanuni bila kutatua kero za msingi ni kazi bure!

    ReplyDelete
  7. Sasa ikiwa kocha hiyo suruali aliyovaa siyo ya heshima je wale wachezaji pale uwanjani wengine hushusha bukta zao mpaka kwenye makalio je wale ndio heshima au hamna la kusema nyie tff?

    ReplyDelete
  8. Basi na hao wachezaji waingie uwanjani na suruali

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic