November 4, 2019



RAMADHAN Nswazurimo, Kocha Mkuu wa Singida United amesema kuwa kinachoiponza timu yake kushindwa kupata matokeo kwenye mechi zake ni kushindwa kujiamini kwa washambuliaji wake.

Singida United ikiwa imecheza juma ya mechi 10 sawa na dakika 900 imefunga jumla ya mabao mawili pekee huku ikiruhusu kufungwa jumla ya mabao 10 ikijikusanyia pointi nne pekee.

Nswazurimo amesema kuwa wachezaji wake wanashindwa kujiamini wakiwa na mpira jambo linalowafanya washindwe kufunga licha ya kuwa na nafasi nyingi ndani ya uwanja.

“Nimegundua kwa sasa tatizo kubwa kwa washambuliaji wangu ni kushindwa kujiamini wakiwa na mpira ndani ya eneo la hatari hata wakiwa nje ya 18 wanashindwa kufanya maamuzi.

“Tayari nimegundua namna bora itakayowarejesha kwenye ubora na kwa kuanza nitaanza kuwajenga saikolojia yao ili wawe makini katika umalizaji wa nafasi ninaamini tutafanya vizuri,” amesema Nswanzurimo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic