November 4, 2019



HITIMANA Thiery, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kinachomkwamisha kupata matokeo kwa sasa ugenini ni kuwa na majeruhi wengi ndani ya timu yake jambo linampasua kichwa kwenye upangaji wa kikosi.

Namungo FC ambayo imepanda ligi msimu huu imeshindwa kufurukuta kwenye mechi zake zote tatu za ugenini kwa kuruhusu vichapo huku ikikaza ikiwa nyumbani kwa kujikusanyia jumla ya pointi 13.

Namungo imepoteza jumla ya pointi tisa ugenini ilianza mbele ya KMC kwa kukubali kuchapwa bao 1-0 kisha ikafuata mbele ya Azam FC kwa kufungwa mabao 2-1 kabla ya kupoteza mbele ya Kagera Sugar kwa kufungwa mabao 2-0.

Ikiwa uwanja wa Majaliwa, Namungo haijapoteza mchezo hata mmoja kati ya mitano iliyocheza na iliambulia sare moja ya bila kufungana mbele ya Mwadui FC na kushinda mechi zote nne mbele ya Ndanda FC mabao 2-1, Mtibwa Sugar bao 1-0, Lipuli bao 1-0 na Singida United kwa mabao 2-0.

Akizungumza na Saleh Jembe, Thiery amesema kuwa mechi nyingi za ugenini amekuwa akichezesha wachezaji wake wengi wakiwa ni majeruhi jambo linalomnyima matokeo.

“Kwa sasa kikosi changu hakipo sawa wachezaji wangu muhimu ni majeruhi na nimekuwa nikiwachezesha baadhi kutokana na kukosa mbadala wake kwa mfano Lukas Kikoti mbele ya Kagera Sugar nilimpanga pamoja na Bigirimana Blaise.

“Kwa sasa tunaangalia namna wachezaji watakavyoamka kwani tuna mchezo dhidi ya Ruvu Shooting na tutakuwa nyumbani tunaomba mashabiki watupe sapoti,” amesema.


1 COMMENTS:

  1. Mbona nyumbani wanashinda? Au wakicheza nyumbani hao majeruhi wanapona ghafla na kupata matokeo?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic