December 9, 2019





ILIKUWA miaka, miezi, wiki na juzi Jumamosi ikafikia ile siku muhimu kwenye soka la Tanzania, ndiyo, ni Klabu ya Simba kuzindua viwanja vyao viwili vya mazoezi vilivyopo Bunju jijini Dar. Hongera sana kwao, tunajivunia wao.

Simba ina miaka zaidi ya 80 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1936 kwa miaka yote haikuwahi kuwa na uwanja wao wa mazoezi tu, ililazimika kulipia Sh 500,000 kwenye viwanja vya kukodi ili wachezaji wapata nafasi ya kufanya mazoezi.
Ilikuwa aibu sana kwao, na walitumia gharama kubwa kulipia fedha kwa ajili ya kufanya mazoezi tu, lakini pongezi kubwa kwa mfumo waliouchagua ambao leo hii unaleta matunda.

Simba iliamua kuingia kwenye uendeshaji klabu kwa mtindo wa hisa, mwekezaji mkuu, Mohammed Dewji ‘Mo’ alichukua hisa 49% na klabu imebakiwa na 51%, hapa mageuzi ndipo yalipoanzia.

Baada ya hapo, Simba wakafanikiwa kurejea kwenye viwango vyao na kurejesha mataji mawili ya ligi kuu kisha wakafanya kweli kimataifa baada ya kucheza hadi robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, haya ni mafanikio ya kujiendesha kisasa.

Ukiachana na hilo, pia wamefanikiwa kujenga viwanja vyao viwili vya mazoezi, kimoja cha nyasi asilia na kingine cha nyasi bandia, hapa itetegemea na kocha anataka kufanya mazoezi kwenye uwanjani upi, kongole kwao tena.

Na ukiangalia hili limewezekana baada ya kuachana na ule mfumo mmoja wa kuongozwa na wanachama halafu wanachagua mwenyekiti au rais ambaye anakuwa hana malengo sahihi na klabu.

Tuliona awali wakati wa mfumo wa uanachama pekee, walipita viongozi kadhaa ndani ya timu hiyo na kwenya kampeni walitumia maneno matamu ya kuwadanganya wanachama wao ili wawape kura lakini mwisho wa siku hakukua na maendeleo.

Kila kiongozi aliyeingia madarakani aliona kama ni kitu kigumu sasa chini ya Mo Dewji naona hili limewezekana, kumbe kila mtu akiamua inawezekana, tufanye kazi tuache maneno.

Angalia leo hii hata wapinzani wao, Yanga nao wameanza mchakato mdogomdogo lakini naona wazi kama itachukua muda mrefu kukamilisha kile ambacho wamepanga kukifanya hii ni kutokana na mfumo uliopo.

Wanapaswa kubadilika, wasione kama wanaiga, ngoja niwaambie, kuiga maendeleo ni kawaida sana tena mnaweza kufanya vyema zaidi ya wale waliotangulia.

Ni aibu mpaka leo hii klabu hizi kongwe kuonekana zinashtuka sasa lakini kwa kuwa Simba wameshafanya tunawapongeza na sasa kazi ihamie kwa Yanga kwani wao pia ni kama kioo kwa timu zingine kibao zinazochipukia.
Ni aibu kila siku kukodi viwanja kwa ajili ya mazoezi tu, ni aibu kubwa sana. Yanga ina mtaji mkubwa, inapaswa kubadilika na kujiendesha kisasa. Mpira wa sasa ni fedha na hilo halikwepeki.

Kama utakumbuka kipindi Yanga ipo chini ya mwenyekiti Yusuf Manji ilikuwa na wachezaji waliowahitaji, fedha kwao haikuwa tatizo kama ilivyo sasa hivi, sasa Wanajangwani wakubali wakatae wanahitaji mtu wa aina hiyo ili kurejea kwenye mstari wao. Nitarejea panapo majaaliwa.

1 COMMENTS:

  1. Ni muhimu Kumpata muwekezaji mwenye sifa kama sole za Mo ambae ana mapennzi na Simba tangu hapo utotoni na uwezo wa kimali
    sio ambae anatafuta penye lengo la kumtajirisha bila yakuwa na lengo la mapennzi na timu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic