KWANZA
kabisa napenda kuipongeza Serikali yetu iliyo chini ya Rais Dk John Magufuli
kwa hatua mbalimbali za awali za kujihadhari na maambukizi ya Ugonjwa wa Covid-19
unaosababishwa na Virusi vya Corona, ambavyo tangu kulipuka kwake vimekuwa
janga ambalo limebadilisha mustakabali mzima wa maisha ya binadamu duniani kwa
sasa.
Hatua ya
kuamua kusitisha kwa muda wa siku 30 mikusanyiko yote hasa ile isiyokuwa na
ulazima iliyotangazwa na Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ni
ya kupongezwa kwani kama ambavyo tumesikia moja kati ya njia ambazo ugonjwa huu
husambaa ni kupitia hewa.
Pili napenda
kuipongeza TFF na Bodi ya Ligi kwa utekelezaji wa maazimio hayo ya Serikali kwa
kuamua kusitisha michezo ya ligi zote ambazo ziko chini ya TFF na bodi hiyo kwa
siku 30 hii ni hatua nzuri katika mapambano haya dhidi ya Corona na inastahili
pongezi.
Baada ya
maamuzi haya ya TFF na Bodi ya Ligi tumesikia kuwa klabu nyingi zimelazimika
kuvunja kambi zake na kuruhusu wachezaji wao ‘wakajikarantini’ majumbani mwao
huku wakisubiri taarifa mpya kutoka TFF hasa baada ya hizi siku 30 kuisha.
Swali kwa
klabu zetu ni kuwa baada ya kuvunja kambi je, wamewaruhusu wachezaji hao kutoka
nje ya mipaka ya Tanzania? Na kama wamewaruhusu je, huko waendako ni sehemu
salama? Na je, ni tahadhari gani ambazo wanazichukua wakiwa huko?
Ni muhimu
kuuliza maswali haya kwani tumesikia baadhi ya wachezaji wa kigeni tayari
wameondoka na wako nje ya nchi kwa maana wamerudi nchi zao za asili.
Wachezaji kama
Meddie Kagere wa Simba inaelezwa yuko kwao Rwanda na David Molinga, straika wa
Yanga inaeelezwa kuwa yupo Ufaransa.
Kumekuwa na
hofu juu ya majaliwa ya wachezaji hawa na hata baadhi ya makocha katika suala
la wao kurudi nchini hasa baada ya TFF kupitia kwa Rais wake, Wallace Karia
kutoa tamko kuwa nyota hawa hawataruhusiwa kurudi nchini, hapa ipo haja ya
hekima kutumika katika suala hili.
Tunatambua kweli
lilitolewa zuio la wachezaji kutotoka nje ya nchi lakini hao tayari wamekwenda
kwao, kwa hiyo kama itatokea wakirudi basi hekima itumike kwa kuwapima na
kuwaweka karantini kwa ajili ya kuzuia maambukizi kwa wenzao.
Mwisho
kabisa napenda kuwakumbusha wachezaji wanaokipiga katika klabu mbalimbali
nchini kukumbuka kuwa wapo vitani hivyo likizo hii ya ghafla isiwafanye
wakajisahau na kwenda kuponda raha bila kufanya mazoezi ili kuendelea kujiweka
fiti.
Kwani kama
wataangukia katika mtego huo wa kula bata bila matizi ni dhahiri kuwa watakuja
kuzigharimu klabu zao pindi Ligi itakaporejea.
Lakini kwa
nafasi ya pekee sana tuendelee kuwakumbusha wachezaji wetu ambao walikuwa
katika kambi ya Taifa Stars kuwa bado nchi inaendelea kuwategemea.
Hivyo likizo
hii iwe sehemu ya kuongeza utimamu wao wa mwili kama ambavyo kocha Ettiene Ndayiragije
amewaagiza na atakayekiuka ni dhahiri kuwa atapoteza nafasi yake.
Umeongea vizuri hasa wachezaji waliokwenda makwao nje ya nchi. Wakirudi hekima itumike kama walivyo wasafiri wengine wanapoingia nchini, wapimwe, waingie kwenye karantini siku 14 baada ya hapo wawe huru kutumikia vilabu vyao. Wapo Meddie Kagere, David Moringa, Kocha Luc wa Yanga aliyeenda kuoa kwao Ubeligiji, na wengineo pia. Uongozi ni busara sio kukurupuka kutoka kuwaadhibu wasicheze tena ligi. Kwanini mbona mwongozo wa Serikali upo vizuri tu? TFF
ReplyDelete