KOCHA wa zamani wa Tottenham
Hotspur, Mauricio Pochettino anatamani kuona siku moja
anarejea katika klabu ya Newell's Old Boys
akiwa na staa wa Barceona Lionel Messi.
Pochettino ambaye ni raia wa Argentina aliwahi kuichezea
klabu hiyo wakati anaanza soka kama ambavyo Messi naye ameanzia soka
katika klabu hiyo.
“Matumaini yangu ni kuona siku moja narejea katika klabu ya Newell's Old Boys naona kama
nachelewa lakini itakuwa ndani ya miaka 10 ijayo, ila nitakuwa na
Messi.
Pochettino alisema kuwa matumaini yake makubwa
yako hivyo lakini anaamini kuwa Messi atacheza hata Kombe la Dunia
lijalo.
“Messi atacheza Kombe la Dunia Qatar 2022 na atafanya
vizuri bila kujali umri wake atapambana tu, unajua uwepo wake ndani ya timu ni
kitu kikubwa sana ataipambania tu Argentina kwenye michuano hiyo," amesema.
0 COMMENTS:
Post a Comment