ILIKUWA mwezi, wiki, hatimaye sasa ni siku moja imebaki kabla ya dunia kushuhudia ile dabi ya Kariakoo. Watani wa jadi Yanga na Simba wanatarajiwa kukutana Novemba 7.
Kila mdau na
shabiki kwa sasa ni mshindi kwa kuwa anaona namna wachezaji wake wanavyopambana
ndani ya uwanja kusaka matokeo.
Kwenye mechi
zao ambazo zimepita kila kitu kipo wazi na ninaamini kwamba maandalizi ya timu
zote mbili yapo vizuri suala la kupeperuka tena dabi mwezi huu hilo inaonekana
hakuna tena.
Awali ilitarajiwa kuchezwa Oktoba 18 Uwanja wa Mkapa ila mambo yalibadilishwa na Bodi ya Ligi Tanzania,(TPLB) kwa kile ilichoeleza kuwa hofu ya usafiri kwa wachezaji ambao waliitwa kwenye timu zao za taifa.
Kikubwa
ambacho kinatakiwa kwa mashabiki ni kuwa watulivu na kuwaacha walimu wafanye
yao ila wao jukumu lao ni moja tu kujitokeza uwanjani kuzipa sapoti timu, basi
hakuna kingine.
Wachezaji
wakati wenu huu sasa kushusha presha kwa mashabiki. Ugonjwa wa mashabiki ni
kuona mpira mzuri achana na pira gwaride ama pira kashata weka pembeni mpira
mzuri unahitajika.
Masuala ya ugomvi
ndani ya uwanja kwa kuwa ni dabi kwa wachezaji tupa kule chezeni mpira ndicho
ambacho kinawafurahisha mashabiki kisha mkicheza kwa ustaarabu matokeo
yatakayopatikana yatawafanya mashabiki kuwa na furaha.
Utamaduni wa
Tanzania namba moja ni upendo hivyo ninaamini kwamba hakutakuwa na ugomvi
kuanzia kwa mashabiki na wachezaji pia. Utulivu unahitajika wakati wa kuzipa
sapoti timu hizi mbili ambazo ni timu pendwa.
Pia kwa
mashabiki kwa wakati huu hamtakiwi kubeba matokeo mfukoni na kuamini kwamba
yatatokea, hilo jambo nakushauri ndugu yangu, rafiki yangu futa kabisa
akilini mwako.
Kwa mwendo
wa ligi hii, mwenyeji anapigwa na mgeni pia anapigwa hivyo sio mwenyeji mwenye
uhakika wa ushindi wala mgeni mwenye uhakika wa ushindi, dakika 90 zitaamua
nani ni nani.
Waamuzi pia
kwa sasa mna wimbo wenu mpya ambao mpo nao kwa wakati huu kazi ni kwenu sasa
kuuimba kwa uzuri wimbo wenu wa sheria 17.
Hakuna
mtihani mgumu kwa wakati huu kuchezesha dabi ambayo inafuatiliwa na dunia
nzima. Umakini unahitajika na sheria 17 muhimu kufuatwa.
Ikitokea
mwamuzi akaboronga ni rahisi kuzomewa ama kusababisha vurugu jambo ambalo
hakuna Mtanzania anayependa kuona tunafikia hatua hiyo.
Masuala ya
kuboronga makusudi kwa kuwa kuna adhabu eti za kufungiwa ama kuonywa hilo
lisipewe kipaumbele muhimu kufuata sheria 17 za mpira.
Ninaona
wachezaji wapo ambao wamepania kufanya maajabu, kikubwa ni maandalizi kwa timu
zote kuanzia benchi la ufundi, wachezaji wenyewe wanapaswa waache matokeo yao
nyumbani na kuamini kwamba matokeo yatapatikana ndani ya dakika 90.
Kila timu na
ifanye kazi katika kufanya maandalizi mazuri na kuweka saikolojia za wachezaji
katika usawa ili kuondoa zile presha.
Matukio
mengi yamekuwa yakitokea na kufanya wengi wasiamini matokeo ambayo yatatokea,
mpira una mambo mengi, tukutane Novemba 7.
Mashabiki ni muhimu kuwa watulivu na kuzipa sapoti timu zenu ndani ya uwanja kuona burudani itakavyokuwa.
Wachezaji mna kazi ya kutoa burudani kwa kucheza vizuri mpira uwanjani zile butuabutua hazipaswi kupewa nafasi bali utulivu kwa kila timu kutawafanya mzidi kuwa imara.
Jambo jingine ni kwamba mchezo huu ni fursa kwenu kujiweka kwenye orodha ya wachezaji ambao wataingia sokoni kwa wakati ujao.
0 COMMENTS:
Post a Comment