February 20, 2021

 BAADA ya beki wa kulia wa timu ya AS Vita Club ya DR Congo, Shabani Djuma kuwasumbua Simba katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya mabingwa Afrika uliofanyika DR Congo, hatimaye uongozi wa Klabu ya Simba umeanza mazungumzo na mchezaji huyo kwa ajili ya kuhitaji huduma yake.




 

Beki huyo wa kulia ni mmoja wa manahodha wa kikosi cha AS Vita ambapo licha ya kuwa ni beki wa kulia lakini ndiye kinara katika utupiaji wa mabao katika kikosi cha AS Vita katika Ligi Kuu ya Congo mara baada ya kufunga mabao matano katika ligi hiyo msimu huu huku akiwapita baadhi ya washambuliaji wa timu hiyo.




Mmoja kati ya wachezaji wa kikosi cha AS Vita ambaye ni rafiki mkubwa wa beki huyo ambapo wote walicheza katika mchezo dhidi ya Simba, amesema kuwa ameambiwa na mchezaji huyo viongozi wa Simba wameanza kuulizia uwezekanao wa kumsajili mchezaji huyo mwisho wa msimu huu.

 

“Djuma ni rafiki yangu, tumekuwa wote AS Vita kwa muda sasa na wote ni manahodha katika kikosi hiki, ameniambia kuna viongozi wa Simba wanamfuatilia kwa ajili ya uwezekano wa kusajiliwa mwishoni mwa msimu huu, sijajua yeye kwa upande wake ataamua nini na anafikiria nini kuhusu Simba,” alisema kiungo huyo.

 

Simba licha ya kumuhitaji beki huyo ambaye anacheza upande wa beki wa kulia, katika nafasi hiyo wapo Shomari Kapombe na David Kameta ‘Duchu’.


Lemgo kubwa ni kuongeza nguvu kwa upande wa beki ili kuongeza nguvu sehemu ya ulinzi kuwa imara zaidi hasa kwenye mechi za kimataifa ambazo ushindani wake ni mkubwa.



16 COMMENTS:

  1. Kijana anaujua mpira haswa ,,aje tu msimbazini.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Shabani ni mchezaji haswa ila sidhani kama wanaweza kushindana na vilabu vyenye nguvu zaidi ndani na nje ya bara la Africa kuipata saini yake. Ni mchezaji klabu yeyote ya Africa yenye malengo ingetamani kuwa nae hata kwa record signing fee.

      Delete
  2. Mmeshaanza kumrubun, nawashaur as vita wasimpange tena huyu beki itakuwa kama kwa chikwende sasa

    ReplyDelete
    Replies
    1. Visingizio FC AKA malalamiko FC Kila wanachotaka kufanya Simba lazima walalamike Yani tumrubuni kwa lipi hasa tumecheza nao kwao uwanja wao ambao hawajafungwa karibu mwaka mzima tumewafunga tuje kumrubuni akija hapo Taifa tatizo washabiki wengi wa Yanga mmekalia propaganda na kuzusha vitu ambavyo havipo ili kuidhoofisha Simba na ndio Mana hamuendelei,nyie endeleeni na propaganda sijui marefa wanawaonea sijui Mara TFF yote Simba,sijui Simba wanacheza mechi zetu so tunazidi kuchanja tu kimataifa nyie bakini hapo hapo kwenye kuwapokea wapinzani wa Simba na kuwatafutia hifadhi

      Delete
  3. Simba ndio timu inayojuwa kuchaguwa nyota wa kazi. Simba huchaguwa kimyakimya bila ya kelele na majigambo kwa kuwaita machine za magoli na nyota wenyewe kudai kazi yetu ni kutia magoli na mwisho wa siku Kumbe hawana chochote. Nyota wa kweli hataki muda wa kuzoweana kama akina Kagere, Konde Boy na wengineo siku ya kwanza Kagere alitia goli

    ReplyDelete
  4. Siku hizi jamaa kimya kuhusu kuleta mashine mpya za magoli na Mnyama mwenyewe anapomtaka nyota ambaye kwahakika arazudu kuipaisha juu timu kutokana na hasadi zao kama wa huyo hapo juu anasema "wameshaanza kumrubuni". Zile harakati zao za kila siku za kuwarubuni wachezaji wa Simba sasa zimekufa Fofofoooo

    ReplyDelete
  5. Hivi huyu beki Shabani Djuma ana umri gani... Anaejua anisaidie

    ReplyDelete
  6. KWA SUALA LA KUVUNJA MKATABA SIMBA ITASHINDWA, AS VITA WAMETUZIDI UCHUMI. KAMA WATAMUWAHI MKATABA WAKE UKIISHA WANWEZA KUMPATA KWA BEI CHEE, LAKINI IATEGEMEA NI TIMU GANI PIA ZIMEPELEKA OFA NZURI KWAKE. HILI SUALA NI KAMA LA WALTER BWALYA. WALTER ALIKUWA MCHEZAJI WA KAWAIDA SANA AND EVEN NOW AKIWA AL AHLY. LAKINI NKANA RANGERS WALIDAI DOLA LAKI 400. NANDIYO HIZO HIZO AL AHLY WALILIPA KWA NKANA RANGERS. AL AHLY WAMEIZIDI SIMBA KWA UCHUMI. KIKOSI CHA AL AHLY KINA THAMANI YA EURO MILIONI 25.5 NI SAWA NA BILIONI 71.66 ZA KITANZANIA.

    ReplyDelete
    Replies
    1. al ahly hawakumnunua bwalya kutoka nkana mzee bwalya kuna timu ya hapo misri ndo ilimsajiri na al ahly ndo wakamchukua

      Delete
  7. Sawa kabisa,Ila mpira Ni uwekezaji na Simba ndo timu pekee Tanzania iliyo na uchumi mzuri kwa Sasa.

    ReplyDelete
  8. Sawa Ila Simba wanaweza kwa sasa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic