KOCHA Mkuu wa Klabu ya Coastal Union, Juma Mgunda amesema kuwa lawama zote za timu yake kupoteza mchezo wowote ule ndani ya ligi zimfikie yeye kwa kuwa ni mpangaji mipango namba moja na anajua pale ambapo wanakosea.
Juzi,
Coastal Union ilikubali kichapo cha mabao 4-0 dhidi ya Gwambina FC ambapo mabao
yalifungwa na Meshack Abraham dk 9,Paul Nonga dk 31, Rajab Athuman dk 37 na
Jimson Steven dk 75 na uwanja huo ulikuwa na maji kutokana na mvua ambazo
zinanyesha kwa sasa.
Akizungumza
na Championi Jumatatu, Mgunda alisema kuwa lawama zote kuhusu kupoteza mchezo
wake ndani ya ligi apewe yeye na sio wachezaji.
“Ninasema
kwamba lawama zote kuhusu kupoteza kwa mchezo nipewe mimi, wachezaji wao
waacheni. Ninasema hivyo kwa sababu ninajukumu la kuwafundisha na waelewe pale
ambapo wanakosea makosa tunayafanyia kazi,” alisema.
Kichapo
kikubwa ambacho Coastal Union ilipokea ndani ya ligi kwa msimu huu ilikuwa ni
pale ubao uliposoma Coastal Union 0-7 Simba, Uwanja wa Coastal Union.
Kwenye
msimamo ipo nafasi ya 13 ikiwa imecheza mechi 24 kibindoni ina pointi 27.
0 COMMENTS:
Post a Comment