July 6, 2021

 


RASMI mabosi wa Yanga wamekamilisha dili lao la kumsainisha nyota wa AS Vita, Djuma Shaban kwa kandarasi ya miaka miwili.


Hivi karibuni Injinia Hersi Said ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Yanga alikwea pipa kuelekea DR Congo ambapo ilielezwa kuwa alimalizana na baadhi ya nyota ikiwa ni pamoja na Djuma.



Picha ambazo zimesambaa leo katika mitandao ya kijamii zimemuonyesha beki huyo akimwaga wino na moja akiwa na Injinia.


Kuhusu usajili wa msimu huu Injinia aliweka wazi kwamba watafanya usajili mzuri ambao utakuwa ni wa kisasa kabisa.


Taarifa zimeeleza kuwa nyota huyo atajiunga na Yanga msimu ujao wa 2021/22 atatambulishwa rasmi siku ya Wananchi.

13 COMMENTS:

  1. Kumbe ilikuwa bado

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kila kitu ni mchakato sio kama kwenda kukata tiketi ya mwendo kasi kisha unasubiri basi lije.

      Delete
    2. MtaMshia michakato kila mwaka wenzenu Wana wanatimiza malengo ya kubeba vikombe

      Delete
  2. Replies
    1. Au fiston, sarpong yikpe, na wengine waliovunja mikataba

      Delete
  3. Hv Jana Chikwende hakuingia kabisa

    ReplyDelete
    Replies
    1. Anasubiri kunyanyua makwapa Mara 2

      Delete
  4. Simba wajinga sana walianza oooh atuwezi kumchukua djuma now wamebadilika kuona kwanza yanga sio wamaneno kama yule msemaji wao sasa nyie jisahau mkazani kila mwaka nguvu ya wachezaji ni ile ile wanapugua kasi na wenzenu tunafanya usajili wa vijana, siku zote usijisifie huna mbio msifie na anayekukimbiza

    ReplyDelete
  5. Mtuboreshee tu kikosi hatutaki maneno mengi.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic