October 10, 2021

 


BONDIA Mtanzania, Dulla Mbabe amepoteza katika pambano lililopewa Kiboko ya Wageni katika pambano la raundi 10 mbele ya Tshimanga Katompa usiku wa kuamikia leo.

Pambano hilo lilikuwa na ushindani mkubwa ilishuhudiwa vitasa vya maana kutoka kwa mabondia hao wawili huku Mbabe akishindwa kuonyesha ubabe.

Katompa raia wa DR Congo alionekana kuzijua mbinu za Mbabe ambapo makonde aliyokuwa anamshushia yalikuwa na ujazo mzito kwelikweli.

Ni ushindi wa pointi ambao Katompa amepata mbele ya mfalme wa Wazaramo, Dulla Mbabe.

Pambano hilo la kukata na shoka lilifanyika katika ukumbi wa PTA Sababasaba na ilikuwa mubashara ndani ya Azam TV.


Inakuwa ni pambano la pili kwa Mbabe kubwa kupoteza kwa kuwa alikuwa ametoka kupoteza lile alilotwangana na Twaha Kiduku.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic