August 29, 2014

MANJI (KUSHOTO) AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO. KULIA NI KATIBU MKUU WA YANGA, BENO NJOVU.


Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji, leo ametoa kali kwenye kikao chake na waandishi wa habari aliposema kwamba ana uwezo wa kuwanuanua wachezaji wa Simba, halafu wasicheze ligi na badala yake wawe wanafanya mazoezi Covo Beach tu.

Manji amesema hayo wakati akipinga Simba kutangaza kumsajili mshambuliaji Emmanuel Okwi.
Manji amesema suala hilo ni sawa na uhuni kwa kuwa Simba inajua Okwi ana mkataba na Yanga.
“Kama itakuwa ni kufanya mambo kwa staili ya kihuni, hata mimi ninaweza kuamua kuwanunua wachezaji wa Simba sijui kina (Amissi) Tambwe na wenzake, halafu wawe wanafanya mazoezi Coco Beach tu, wasicheze ligi.
“Lakini busara ni jambo jema, lakini nione kwamba ninachofanya ni kitu gani na hasara zake ni zipi.
“Umesikia sisi (Yanga) tumelalamika kuhusiana na usajili wa Domayo au Kavumbagu kwenda Azam FC. Kila kitu kilikwenda kwa utaratibu.
“Hata Simba wanaosema kuhusiana na suala la Okwi pia hawajui, sisi hatukuzozana na Simba, utaona Okwi wakati anakuja Yanga tulifuata utaratibu na kumalizana na SC Villa.
“Simba hawakuwa na tatizo na Okwi, badala yake Etoile du Sahel ya Tunisia ambayo Yanga hatukufanya nao biashara. Hakukuwa na sehemu ambayo inatugonganisha,” alisema.
“Sasa kama kuna lengo la kufanya ili kuikomoa au kuona ni kulipa kisasi, basi ni kujidanganya tu na kutaka kufanya mambo yaende kwa kukomoana ambalo si jambo zuri.
“Ndiyo maana tumetoa siku saba tuwaachie TFF washughulikie madai yetu, ikishindikana, Caf, Fifa au Cas bado ni sehemu tunazoweza kwenda,” alisisitiza Manji.
“Pia kusema Okwi amevunja mkataba nasi ni kujidanganya. Iko wapi barua aliyonayo yeye kwamba tumevunja naye mkataba.
“Hata majina tumetuma sita, tungejua lipi la kulitoa kwa kuwa hadi Septemba 6 ndiyo mwisho wa kusajili wageni. Haraka ya nini?”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic