December 13, 2013


Saa chache baada ya Ivo Mapunda kusaini Simba, kocha wa Gor Mahia amesema amesikitishwa na uamuzi wa kipa huyo.
Bobby Williamson amesema hakuzungumza na Mapunda kuhusiana na suala hilo.

“Ningeweza kumshauri zaidi, ni kipa mzuri na nilikuwa namhitaji. Najua siwezi kumzuia lakini ningemshauri,” alisema.
“Nimesikitika, sisi tulitarajia kuzungumza naye mara tu baada ya michuano ya Chalenji, lakini hakuna namna sasa. Zaidi namtakia mafanikio mema,” alisema kocha huyo.
IVO AKIWA MAZOEZINI GOR MAHIA...

Ivo tayari amemwaga wino kuichezea Simba akitokea Gor Mahia ambayo alichangia kuipa ubingwa msimu uliopita ingawa zaidi alikuwa kipa namna mbili.
SALEHJEMBE ilikuwa blogu ya kwanza kuandika kuhusiana na mafanikio makubwa ya Ivo nchini Kenya.

Moja ya gumzo ni taulo yake ambayo ilipata umaarufu mkubwa na hasa kutokana na uwezo wake wa kupangua mikwaju ya penalty.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic