September 21, 2014

Baada ya kuongoza kwa mabao 3-1, Man United imejikutwa ikichapwa mabao 5-3 na Leicester City.
Katika mechi hiyo ya ugenini ya Ligi Kuu England, Man United ilianza kupata mabao yake kupitia kwa van Persie, Di Maria na Ander Herera.
Lakini taratibu Leicester wakaanza kurudisha kama utani.

Alianza Leonardo Ulloa, akafuatia David Nugent, mkongwe Cambiaso halafu Jamier Vardy kabla ya Ulloa kumaliza kazi kwa penalti tena.
Kocha Louis van Gaal na msaidizi wake, Ryan Giggs walionekana hawaamini kilichokuwa kinatokea.
Beki Blackett wa Man United ambaye alionekana kuchemsha zaidi, alilambwa kadi nyekundu.









0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic