October 1, 2020


 KLABU ya Yanga imeibua upya utata mwingine wa mkataba wa mshambuliaji Bernard Morrison wakidai hana mkataba halali na mabosi wake wa sasa ambao ni Simba.

 Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela amesema hayo leo Oktoba Mosi kwa kueleza kuwa wakati klabu yao ikipokonywa haki ya umiliki wa Morrison wamebaini mapungufu makubwa katika mkataba wa mchezaji huyo na Simba.

 

Mwakalebela ambaye amekuja na nakala anayodai ni ya mkataba huo amesema sehemu zote za mkataba huo zimesainiwa na mchezaji huyo pekee hatua ambayo sio sahihi.

 

Amesema katika mkataba huo pia hauna sehemu iliyosainiwa na kiongozi yoyote wa bodi ya Simba lakini pia hauna saini ya shahidi.

 

Pia,amesema katika kila nakala imesainiwa na Morrison pekee bila ya upande wa pili hatua ambayo inaoonyesha watani wao hao hawakuridhia mkataba huo.

 

“Una mapungufu makubwa katika sehemu mbili…hakuwa na shahidi lakini amesaini kwenye upande wake, CEO wa Simba hajasaini. Simba SC haijaridhia mkataba wa Morrison kwa sababu hakuna sehemu yoyote ambapo klabu ya Simba imesaini mkataba wa Morrison.

 

"FIFA inamtambua Morrison ni mchezaji wa Yanga. TMS ya FIFA inamtambua Morrison mchezaji wa Yanga. Mkabata wa Simba na Morrison una dosari, upande wa mchezaji umesainiwa bila shahidi,”  amesema Makamu Mwenyekiti Yanga, Fredrick Mwakalebela.


 Usajili wa Morrison kutoka Yanga kuibukia Simba umekuwa na sarakasi nyingi tangu awali ambapo mwanzo kulikuwa na mvutano mkubwa kati ya mchezaji na mabosi wake wa Yanga.


Yanga walikuwa wakieleza kuwa mchezaji huyo ana dili la miaka miwili huku mchezaji akieleza kuwa ana mkataba wa miezi sita na umemalizika.


Utata huo ulifanya suala hilo kutinga makao makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambapo kesi yake iliskilizwa kwa muda wa siku tatu mfululizo na hukumu ilitolewa kwamba Morrison ni mchezaji huru kwa kuwa mkataba wake na Yanga ulikuwa na mapungufu.


Kwa sasa limeibuka tena sakata hili ambalo nalo linaeleza kuwa bado Morrison mkataba wake ndani ya Simba una mapungufu muda ambao dirisha la usajili limefungwa na mchezaji huyo akiwa ameshacheza mechi ndani ya Simba.


17 COMMENTS:

  1. Kwa hiyo TFF wamemtambua vipi na kumruhusukuchezea simba au ndio mwasho wa tarehe 18/10. Unataka kuwapoteza simba wenzako wana bodi ya usajili sio kama nyinyi

    ReplyDelete
  2. Hao yanga wamechanganyikiwa tu na Morrison,wanawaza tar 18 itakuwaje, mkataba wa Simba na Morrison unawahusu nn wao yanga,mchezaji ndo huwa analalamika juu ya mkataba wake,Simba inawachezaji 30 hakuna mchezaji alielalamika kuhusu mkataba wake,,,Sasa hao yanga wanahangaika kuchunguza mikataba ya wachezaji wa timu nyingne inawahusu nn,unahangaika na mke wa mtu kujua Kama mme wake amesain cheti Cha ndoa au hajasain,ili iweje

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inawezekana ndio nyaraka alizowapelekea senzo

      Delete
    2. Hizo nyaraka zipo CAS na siyo Senzo. Kwani Senzo ndio anamiliki CAS? Endeleeni na ushabiki ila hili jambo ni gumu sana kwa Simba na wakizubaa watanyang'anywa points zote katika mechi Morison alizocheza

      Delete
    3. Ndio mnavyodanganywa mtazidi kupata stress

      Delete
    4. Viongozi wa Simba ebu fukueni ile sakata la Mwakalebela kuongea na chama ilihali akiwa na mkataba...anawashwa huyu anahitaji kukunwa vizuri tarehe 18/10

      Delete
    5. Hivi Kwa akili zenu unafikiri Simba wanakurupuka hawana wanasheria?

      Delete
  3. Utopolo Senzo anawapoteza msije juta, toeni matokeo ya CAS acheni blaablaa. Mmeshaliwa na GSM mmeliwa tu.

    ReplyDelete
  4. Hii sasa inaitwa danganya toto. Kama mkataba haujasainiwa na simba huyo morisson angekubali vipi kucheza simba bila mkataba ili hali anajua kilichomtokea yanga? Mikataba yote ya wachezaji wa yanga anasaini gsm, kwani ndio kiongozi wa yanga?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Haiingii akilini kabisa. TFF ingemruhusuje mchezaji kuchezea Simba kama mkataba ulikuwa na mapungufu? Morrison angepataje kibali cha kazi kutoka wizara husika bila mkataba uliokamilika? TFF ndiyo iliyoondoa jina la Morrison kwenye orodha iiyopelekwa TFFna Yanga na badala yake likabakia Simba. Hii ni baada ya kujirishisha document muhimu zote za mchezaji zilishakamilka kikiwepo kibali cha kazi

      Delete
  5. Yanga mnataka point Simba anyang'anywe ili mchukue ubingwa kwa makando kando kweli nyie makando kando fc chezeni mpira mnazalilisha wachezaji wenu kuonekana si kitu mbele ya Morrison basi wapeni ubingwa yanga tff na ligi iishe basi

    ReplyDelete
    Replies
    1. True, uwanjani wanechemka wanataka ushindi wamezani.

      Delete
    2. Magori kawajibu vizuri mkataba unawahusu Simba, Morison, FIFA na tff wao yanga huo mkataba wameupataje

      Delete
  6. Mwakalabela akimaliza atuambie tonombe na yule nyoshi wamewasajili au wapo kwa mkopo. Yanga wamekuwa wanasheria

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic