October 1, 2014


Na Saleh Ally
VIGUMU kuamini kama Kocha Arsene Wenger amekitengeneza kikosi chake katika ubora wa juu na kinaweza kuwa ni kati ya vikosi vyenye nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa England.

Inakuwa ni vigumu kwa wengi kuamini kweli kikosi cha Arsenal kinaweza kubeba ubingwa kwa kuwa kimekuwa kikianza vema na mwishoni kuishia kugombea nafasi ya nne au tatu.

Hata hivyo, kitendo cha kutwaa ubingwa wa Kombe la FA msimu uliopita kinaonyesha imani ya mashabiki wake inaweza kupanda na hadi ligi imechezwa mechi 120, yaani kila timu mechi sita, Arsenal inaonekana iko kwenye takwimu za juu katika timu zinazomiliki mpira vema.

Inawezekana timu ikamiliki mpira sana lakini isifanye vizuri, lakini kiufundi hata aina mpya bora ya ulinzi ni timu kumiliki mpira mwingi kwa kuwa ukiwa nao, hakuna anayeweza kukupokonya.

Ukiachana na umiliki wa mpira, Arsenal ndiyo timu inayoongoza kwa kuwa na pasi nyingi zaidi zilizofika katika mechi hizo 120 za Premier League zilizopigwa msimu huu.

Ina asilimia 87.2 ambayo ni ya juu zaidi na hii ni silaha nyingine, kwamba timu inayofikisha pasi nyingi sehemu sahihi inakuwa na nafasi nzuri ya kufanya vizuri kwa kuwa inatekeleza kilicho sahihi katika mipango yake.

Kama timu itakuwa inapoteza pasi nyingi, maana yake inajiondoa kwenye reli au inajitoa kwenye mipango sahihi inayolenga kufanya.

Unaweza kusema ni kawaida Arsenal kumiliki mpira sana na kupiga pasi za uhakika zaidi, lakini katika mechi hizo 120, Arsenal iko kwenye moja ya timu zinazocheza soka la kibabe.

Arsenal inashika nafasi ya pili kwa timu ‘zinazochafua’ mchezo, kwani tayari vijana hao wa Arsenal Wenger wana kadi 16 katika mechi sita. Wanaoongoza ni Man City wakiwa na 17, utaona tofauti ilivyo ndogo.

Kinachovutia zaidi, Arsenal ina mchezaji katika listi ya wachezaji wababe ndani ya mechi 120. Calum Chambers ndiye anaongoza kundi la wachezaji wenye kadi nyingi, ana nne.

Hii inaonyesha sasa kuna mabadiliko makubwa kwa Arsenal, kwamba wana uwezo wa kucheza mechi kwa aina zote. Pasi na urembo mwingi lakini ikishindikana basi ‘wanakichafua’ na kucheza kibabe.

Mashabiki wa Arsenal wa Tanzania wamekuwa na hofu kama wengine duniani, wanaiamini timu yao, tatizo ni inavyomaliza. Kwa mabadiliko haya ya mapema, kunaweza kuwa kitu kipya, endelea kufuatilia.



UMILIKI WA MPIRA:
Arsenal            63.9%
Man Utd              60.3%
Everton            59%
Man City            58.9%
Newcastle            56.2%


PASI ZILIZOFIKA:
Arsenal            87.2%
Man City            86.6%
Man Utd            86.5%
Chelsea            85.5%
Everton            85.1%

PASI ZA MABAO:          
Cesc Fàbregas                   Chelsea               6
Gylfi Sigurdsson               Swansea             4
Stephen Quinn                  Hull                      3
Jason Puncheon               Crystal Palace   3
Stewart Downing              West Ham           3


VIKOS VIBABE:                      
Man City            17
Arsenal              16
West Ham          14
Swansea             11
Hull                      12


WACHEZAJI WABABE:                                  
Calum Chambers            Arsenal                  4
Jason Puncheon             Crystal Palace      2
Tyler Blackett                  Man Utd                2
Wayne Rooney                 Man Utd                 2


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic