Siku chache
baada ya kufungiwa kujihusisha na soka kwa miaka saba, Damas Ndumbaro ambaye
kitaaluma ni wakili, ametamka kwa kujiamini: “Nilikaa kimya makusudi, sasa
wakati muafaka umefika kuzungumzia hilo.”
Dk Ndumbaro ambaye
alifungiwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana
na kudaiwa kukiuka kanuni kadhaa za soka, anajiandaa kuweka wazi msimamo wake
kuhusu adhabu aliyopewa, saa 5 asubuhi leo Ijumaa.
Dk Ndumbaro amesema kuwa amejipanga kupambana kwa hoja na kamati
hiyo iliyo chini ya Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi.
“Nilibanwa na
majukumu, pia sikupenda malumbano, ndiyo maana nikawa kimya, taarifa zao
nilizipata muda mrefu sana.
“Kesho njoo
kwenye mkutano wangu nitazungumza kila kitu, maana unajua walitoa maamuzi
nikiwa sipo, sasa muda umefika wa kufunguka,” alisema Ndumbaro.
0 COMMENTS:
Post a Comment