October 23, 2014

 
KIKOSI CHA MWADUI KINACHONOLEWA NA JULIO.
Kocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema ushindi wa mabao mengi kuanzia matano ndiyo kitu anachotaka.

Mwadui ambayo ilikuwa imekwenda sare mfululizo kwenye mechi zake za Ligi Daraja la Kwanza iliibuka na kuichapa Polisi Mara kwa mabao 5-1.
Mwadui ndiyo ilikuwa inacheza nyumbani kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga kwa mara ya kwanza msimu huu.
Julio amesema angefurahi kuona kikosi chake kinashinda kwa idadi hiyo ya mabao.
“Mabao matano ikiwezekana zaidi yana faida kubwa. Sema kwenye soka hauwezi kwenda hivyo moja kwa moja.
“Kikubwa ni kwamba tunahitaji ushindi kwa ajili ya kujiwekea mazingira mazuri ya baadaye,” alisema Julio.
Beki huyo wa zamani wa Simba, aliwapongeza wachezaji wake kwa kuonyesha soka safi na kufunga idadi nzuri ya mabao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic