October 2, 2014


Kocha wa Simba, Patrick Phiri amesema yeye na benchi lake la ufundi wanaumiza kichwa sana ili kubadilisha mambo kadhaa.

Phiri raia wa Zambia amesema yeye na wenzake wamekuwa wakifanya kazi kwa nguvu kurekebisha mambo.

"Kuanza kuamini sasa Simba imefanya vibaya haitakuwa sawa, lakini kuamini tunachofanya sasa ni sawa, pia sio sahihi.
"Ndiyo maana tunafanya kazi kwa juhudi kubadilisha hali hii na imani ni kubwa tutabadili mambo na kuanza kufanya vema.
"Hakuna anayeweza kufurahia hali hii, mashabiki na viongozi lakini si hali nzuri kwetu. Hivyo tunaendelea kupambana," alisema Phiri ambaye ni mtaratibu.
Simba imecheza mechi mbili za mwanzo za Ligi Kuu Bara na kutoka sare mbili.

Hali hiyo inaonekana kuwaudhi mashabiki wa Simba na wengi wao wamekuwa wakitamani kuiona angalau inapata ushindi wa kwanza kwenye Ligi Kuu Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic