February 28, 2015


Mkakati wa kumkatia rufaa bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Cheka, bado unaendelea ambapo kwa sasa faili la hukumu ya kesi yake linatarajia kutua jijini Dar katika Mahakama ya Rufaa siku yoyote.


Cheka anatumikia kifungo cha miaka mitatu baada ya kupatikana na hatia ya shambulio la kudhuru mwili dhidi ya meneja wa baa yake, Bahati Kibanda, lililofanyika Julai 2, mwaka jana.

Mmoja wa memba wa familia ya Cheka amesema mchakato wa kumkatia rufaa unaendelea vizuri ambapo muda wowote faili la hukumu ya kesi yake litawasili jijini Dar.

“Kwa upande wetu mchakato wa rufaa tumeukamilisha ambapo kwa sasa kilichobaki ni faili la hukumu ya kesi yake kutua jijini Dar katika Mahakama ya Rufaa.


“Mwanasheria aliyeteuliwa tayari ameshatueleza kuwa tusiwe na wasiwasi, zaidi ni kumuomba Mungu ili kila kitu kiende sawa, kwa maana hiyo lazima Cheka atahamishiwa jijini humo kwa ajili ya kuisikiliza tena rufaa ya kesi yake,” kilieleza chanzo hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic