Kipa
Hussein Sharrif ‘Casillas’, hana nafasi katika kikosi cha kwanza cha Simba
lakini kocha wake Goran Kopunovic amempa mbinu za kucheza ‘first eleven’.
Kwa
muda mrefu Casillas alikuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha ya ugoko
aliyoyapata Afrika Kusini wakati Simba ikijiandaa na mechi dhidi ya Yanga,
Oktoba, mwaka jana, hata alipopona hivi karibuni amekuwa hana nafasi kikosini.
Kuhusu
kipa huyo, Kopunovic amesema: “Kwanza Casillas anatakiwa atambue mechi
zilizobaki katika ligi ni chache, akitaka kucheza kikosi cha kwanza, anapaswa
kujituma.
“Kujituma
ndiyo mbinu pekee itakayomfanya Casillas acheze kikosi cha kwanza, kwani
kinyume na hapo hataweza kupata nafasi, maana wenzake wanajitahidi.”
Simba
ina makipa wanne ambao ni Ivo Mapunda ambaye ni namba moja, Manyika Peter
(namba mbili), Denis Richard na mwenyewe Casillas.
0 COMMENTS:
Post a Comment