March 28, 2015


Kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, amekiri ana kibarua kigumu kuhakikisha Coastal Union inafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara tangu alipokabidhiwa mikoba ya James Nandwa aliyetimka.


Katika msimamo wa ligi kuu, Coastal ipo nafasi ya tano ikiwa na pointi 24 baada ya kucheza mechi 20, ikiwa imefunga mabao 14 na kufungwa 14 na mechi ijayo itacheza na Prisons Aprili 4, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Julio amesema anashukuru CV yake inaendelea kukua, lakini kwa sasa ana kibarua kigumu kuhakikisha Coastal inashika moja kati ya nafasi tatu za juu.

“Najua nakuza CV nikiwa na Coastal, lakini hilo litakuja baada ya kufanya kazi ngumu kwa maana ligi ni ngumu na natakiwa kupambana ili nipate matokeo mazuri,” alisema Julio ambaye ni kocha wa zamani wa Simba.


Julio anaifundisha Coastal kwa muda kwani ligi ikiisha atarejea Mwadui FC ya Shinyanga ambayo hivi karibuni aliipandisha daraja hadi ligi kuu. Zipo timu kadhaa zinazomwania Julio lakini mwenyewe amezikatalia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic