April 27, 2015

YANGA BINGWA
FULL TIME
GOOOOOOOO Dk 83, Bantu anafunga bao safi kabisa kwa shuti kali kutoka nje ya 18

Dk 81, Bantu Admini anapiga shuti kali lakini Dida anaruka na kuidaka kwa ustadi

SUB Dk 75, Yanga inamtoa Tambwe na kumuigiza Nizar Khalfan, inamtoa Msuva anaingia.....
Dk 66, Msuva anaifungia Yanga bao saaafi wakati wachezaji wa Polisi wakidhani ameotea...

SUB Dk 60  Poisi wanamuingiza Nahoda Bakari badala ya Meshack Abel
GOOOOOO Dk 59 Tambwe tena, anaifungia Yanga bao safi kwa kichwa baada ya kuiwahi krosi ya Ngassa

Dk 58 Dida anafanya kazi ya ziada kuokoa shuti kali la Kapibe, kidogo inaonekana Yanga wanapinguza nguvu ya mashambulizi



GOOOOOOO Dk 53 Tambwe tena, anafunga bao la pili kwa Yanga baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa baada ya Msuva kupiga shuti kali. Ni bao lake la 13 msimu huu

SUB Dk 47, Polisi wanamtoa Said Bahanuzi wanamuingiza Nicholas Kabipe. Bahanuzi anatoka na kwenda kumkumbatia Kocha wa Hans van der Pluijm
Dk 46, Yanga wanaanza kwa kushambulia lakini Polisi nao wanaonekana wamejiandaa na wanataka kusawazisha kwa kupeleka mashambulizi lakini yanaonekana kuwa dhaifu

MAPUMZIKO
DAKIKA 2 ZA NYONGEZA
Dk 43, Yanga wanaonekana kuumiliki mpira zaidi, lakini kwa pasi fupifupi, huku wakijipanga taratibu na Polisi wanaonekana kutaka kusawazisha
GOOOOOO Dk 40, Tambwe anaifungia Yanga bao la kwanza baada ya krosi safi ya Msuva
Dk 35 Yanga wanapata kona, lakini wanashindwa kuitumia, inaokolewa

Dk 33, Selembe anapata pasi nzuri ya Bahanuzi, mbele ya lango la Yanga anapaisha mpira unakwenda nje

Dk 26 Selembe anajaribu kupiga shuti kali, lakini Dida anadaka kwa ulaini
KADI Dk 23, James Ambrosse analambwa kadi ya njano kwa kuushika mpira kwa makusudi

 Dk 18, Yanga wanafanya shambulizi jingine, mpira wa adhabu uliopigwa na Niyonzima unatua kichwani mwa Tambwe lakini anashindwa kulenga lango, anauwahi Sherman naye anapiga tik tak juuu
Dk 17, krosi nzuri ya Bantu Admini, inatua kichwani mwa Selembe lakini anashindwa kuupiga vizuri
Dk 14, Polisi wanapata mkwaju wa faulo, ndiyo shambulizi lao kubwa la kwanza. Bahanuzi napiga na mpira unatoka nje ya lango, haukuwa na madhara yoyote

Dk 8, kipa wa Polisi anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa kichwa wa Sherman ikiwa ni baada ya ule uliopigwa na Msuva kugonga mtambaa wa panya na kurejea uwanjani.

Dk 4, nafasi nyingine nzuri kwa Yanga, krosi safi ya Msuva lakini mabeki wa Polisi wanaokoa tena

Dk ya kwanza tu, Yanga wanafanya shambulizi zuri, nafasi nzuri anaipata Twambwe, anapiga shuti lakini linaokolewa na kipa.

2 COMMENTS:

  1. YANGA!YANGA!YANGA!

    ReplyDelete
  2. Mwanahabari wetu wanayanga alishasema jamani!Hapana chezea YANGA,ndio habari ya mujini wajemeni.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic