April 1, 2015


Kocha kuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, amemsifu kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Simon Msuva kutokana na kuzifumania nyavu kwenye michezo ya Ligi Kuu Bara inayoendelea.


Msuva kwa sasa ndiye kinara wa kuzifumania nyavu katika Ligi Kuu Bara kwa kuwa na mabao 11, huku akimuacha kwa bao moja mshambuliaji wa Azam, Mrundi, Didier Kavumbagu, ambaye alikuwa anawaongoza kwa muda mrefu.

Kiungo huyo akiwa chini ya Pluijm, amefanikiwa kufunga mabao nane kwenye ligi kati ya 11 huku matatu akiwa ameyafunga wakati timu hiyo ilipokuwa ikinolewa na Mbrazili, Marcio Maximo ambaye alitimuliwa mwishoni mwa mwaka jana.

Endapo Msuva atafanikiwa kuibuka mfungaji bora msimu huu, basi atakuwa ameibakiza nyumbani tuzo ya ufungaji bora ambayo mara ya mwisho mzawa kuichukua ilikuwa ni msimu wa 2011/12 ilipochukuliwa na John Bocco wa Azam, huku kwa misimu miwili mfululizo ikichukuliwa na wageni.

Pluijm amesema: “Tangu niichukue Yanga nimemuona Msuva akifunga mabao mara kwa mara, ni vizuri kwani huwa anafanyia kazi akiwa mazoezini na ndiyo maana akiwa uwanjani hupata ujasiri na kufanya kile kinachotakiwa.


 “Hakika ni mchezaji hatari sana, tena mara nyingi anapolisogelea lango.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic