Timu ya Mtibwa Sugar
ya mkoani Morogoro, imeapa kubeba pointi sita katika michezo yao miwili ya Ligi
Kuu Bara ambapo wanatarajia kucheza leo Jumatano dhidi ya Kagera Sugar na
Jumamosi watapambana na Stand United, michezo yote ikipigwa kwenye Uwanja wa
Kambarage, Shinyanga.
Mtibwa ambayo kwenye
msimamo wa ligi kuu inashika nafasi ya saba baada ya kuwa na pointi 23, itakuwa
na kibarua kigumu kuzikusanya pointi hizo sita huku ikiwa kwenye harakati za
kutaka kumaliza ligi kwenye nafasi nne za juu.
Ofisa habari wa timu
hiyo, Thobias Kifaru, alisema wameenda mkoani humo wakiwa na imani kuwa
watarudi na pointi hizo kutokana na walivyojiandaa.
“Tumejiandaa kurudi
na pointi zote kwani tumejiandaa vya kutosha kuhakikisha tunamaliza ligi tukiwa
ndani ya nne bora, vijana wapo katika ari nzuri ya kuzichukua pointi hizo,”
alisema Kifaru.
0 COMMENTS:
Post a Comment