May 27, 2015


Ile kesi iliyopo kwenye Mahakama ya Kazi jijini Dar ambayo Klabu ya Yanga imewashtaki wachezaji wake Juma Kaseja na Mbrazili, Geilson Santana ‘Jaja’, inatarajiwa kusikilizwa leo Jumatano kwenye mahakama hiyo.


Awali, kesi ya Jaja ilikuwa inaahirishwa mara kwa mara baada ya mtuhumiwa kuwa mbali huku akiomba kupewa muda wa kutuma mwakilishi au kuja mwenyewe ambapo kesho ni hatua ya mwisho na kama mtu kutoka upande wake akishindwa kutokea mahakamani, basi kesi hiyo itasikilizwa kwa upande mmoja.

Jaja anatuhumiwa na Yanga kwa kuvunja mkataba kinyemela ambapo anatakiwa kuwalipa Yanga milioni 57, hali kadhalika kwa Kaseja ambaye alikiuka masharti ya mkataba, anatakiwa kuilipa Yanga milioni 300.

Mwanasheria wa Yanga, Frank Chacha, ameliambia Championi Jumatano kuwa, kuelekea kwenye kesi hiyo, kila kitu kwa upande wao kinaenda sawa na kinachosubiriwa ni wakati ufike ili haki itendeke.

“Kesi ya Jaja baada ya hatua ya usuluhishi kupita, sasa ipo hatua ya maamuzi ambapo kama akishindwa kufika basi tutaiomba mahakama kesi isikilizwe upande mmoja,” alisema Chacha.


Kuhusu kesi ya Kaseja, Chacha alisema ipo kwenye hatua ya maamuzi ambapo hatua ya kwanza kila mtu amewasilisha maelezo ya awali ambapo leo wanakutana kwa ajili ya kupambanisha hoja za mdai na mdaiwa mpaka itakapofikia hatua ya kuletwa mashahidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic