July 7, 2015


Mashabiki mbalimbali wa Simba wameonekana kutoelewa uuzwaji wa mshambuliaji Emmanuel Okwi.


Mashabiki hao wametuma ujumbe mfupi katika blog hii wakionyesha kutofurahishwa kutokana na kuuzwa kwa Okwi.
Simba imemuuza Okwi katika klabu ya Sonderjyske ya nchini Denmark lakini dau lake limeendelea kuwa siri kubwa.

Wengi wao wameonyesha kuwa jambo hilo limekuwa ni la kushitukiza na wanaona Mganda huyo alikuwa msaada mkubwa katika kikosi chao.

“Inawezekana vipi, wakati tunajiimarisha, halafu Okwi ndiyo anauzwa. Huyu ndiye alikuwa mchezaji wetu aliyefanya vizuri msimu iliopita,” alisema Mohammed Said.

Thomas Maganga aliyejitambulisha kuwa mmoja wa mashabiki wa kutupa wa Simba, alisema: “Naanza kuona kama kuna shida, uuzwaji wa Okwi katika wakati huu kama tulikuwa tuna nia ya kujenga kikosi naona si sahihi.”

Asilimia kubwa ya mashabiki hao walionekana kuwa na hofu kuu. Hata hivyo, baadhi yao walisema si jambo baya kumuuza.
“Unajua Okwi ni mzuri lakini msumbufu, hivyo muache aende tu halafu tujipange.”

Kuhusiana na hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe alilitolea ufafanuzi na kusema.
“Wale watu tuliona ofa yao ni nzuri,” alisema bila ya kuitaja.
“Ukiachana na hivyo, Okwi na Simba kuna makubaliano katika mkataba, moja ni hilo suala kwamba akipata timu tumuachie.
Sasa sioni kama kuna tatizo na lazima mjue wachezaji wanakuja na kuondoka,” alisema Hans Poppe..


2 COMMENTS:

  1. Tatizo sio kuondoka, bali kwanini hatutajiwi dau ameuzwa kiasi gani!! Muda wa kufanya hizi club shamba la bibi uishe jamani!!

    ReplyDelete
  2. Mhh mie nimeanza kuwa na wasiwasi na Hans Pope....unauazaje machine kama Okwi na huku unasema tunataka ubingwa?....sielewi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic